MKAZI
wa Gongolamboto, wilayani Ilala, Dar es Salaam, Simon Chibago, amefariki dunia
baada ya kung’atwa na paka aliyekuwa akimfuga nyumbani kwake.
Akizungumza
na BLOGG hiileo, mmoja wa
ndugu wa marehemu, Rajabu Mustafa, alisema tukio la ndugu yao kung’atwa na paka
lilitokea Februari 14, mwaka huu.
“Chibago
alikuwa ana paka mmoja aliyekuwa anamfuga nyumbani kwake, siku hiyo aliporudi
nyumbani alimuona paka akihangaika na kumfuata miguuni akionyesha kuomba msaada,
ndipo alipodhani amepewa sumu, hivyo akaenda kununua maziwa ili ampe,” alisema
Mustafa.
Alisema
Chibago aling’atwa kwenye kidole cha mkono na paka huyo baada ya kutaka kumpa
maziwa.
Mustafa
alisema baada ya kung’atwa, Chibago hakwenda hospitali kupata tiba, bali
aliendelea na kazi zake kama kawaida huku akishindwa kuwaeleza ndugu zake hadi hali
ilipoanza kuwa mbaya.
“Chibago
alianza kupata maumivu makali, hali iliyowafanya siku ya Jumamosi Februari 21,
mwaka huu kumpeleka Hospitali ya Amana na baadaye kuhamishiwa Hospitali ya
Taifa Muhimbili kwa uchunguzi zaidi,” alisema Mustafa.
Mustafa
alisema hata hivyo Jumatatu ya Februari 23, alifariki dunia na walielezwa chanzo cha kifo ni sumu ya
paka huyo iliyosambaa mwilini kutokana
na kuchelewa kutibu jeraha hilo.
Alisema
Chibago alizikwa juzi Alhamisi. Paka huyo pia alikufa siku aliyomng’ata
Chibago.
No comments:
Post a Comment