MWENYEKITI
Wawamiliki wa Magari ya Abiria (Mabasi) Tanzania (TABOA), Ramadhan Mrutu, amesema
matukio ya ajali mchini yanachangiwa na vyombo vya serikali kwa kushindwa kwao
kusima sheria kikamilifu.
Mrutu
alitoa kauli hiyo wakati alipozungumza na wandishi wa habari kuhusu matukio ya
ajali yaliyotokea katika kipindi hiki cha Machi mwaka huu.
Alisema
ajali hizo zimesababisha vifo vya watu wengi huku wengine wakibaki na vilema
vya kudumu.
Mrutu alisema ajali hzo zinachangiwa mambo manne
au matano, kwanza polisi kushindwa kusimamia ratiba, Sumatra kujaza magari
mengi kwenye barabara moja bila kufanya utafiti wa kuona kama yanatosha au la.
Kingine
ni kinachochangia ajali hizo ni kwa
madereva kupenda kwenda mwendo wa kasi, wako baadhi ya wamiliki wanaopenda
magari yao kuwa ya kwanza kule yanako kwenda.
Pia
baadhi ya abiria nao wanachangia ajali hizo kwa kuwataka madereva wakimbie,
wamekufikia hatua ya kuwaahidi madereva kwamba kila atakapopigwa toshi na
polisi asiwe na wasiwasi watazilipia.
Mrutu
alisema ili kukomesha matukio hayo lazima Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi
kavu (Sumatra), kuangalia utaratibu wake wa kujaza magari katika barabara moja
ili yaende sambamba na wingi wa abiria.
“Mfano
Sumatra inapeleka magari zaidi 20 kutoka Dar es Salaam,
yakiondoka saa 12:00, asubuhi kwenda
Mbeya hali hiyo inachangia magari mengi kutojaa abiri hivyo madereva
kukimbizana njiani kwa ajili ya kugombea abiria, matokeo yake ni ajali,”alisema
Mrutu.Mrutu, alisema kama Kikosi cha Usalama
Barabarani kitafanya kazi kwa uadilifu anaamini kuwa ajali hizo zitapungua.
Alisema
kwa vile polisi wameshindwa kufanya kazi zao vizuri wanapendekeza kikosi hicho
kifanyiwe mabadiliko ili waje polisi wengine watakaofanyakazi kwa uadilifu na
hatimaye kuokoa maisha ya Watanzani wanaokufa kutokana uzembe wa watu wacheche.
Alisema
kama serikali itaamua kudhibiti ajali hizo, inaweza tena kwa kuwatumia polisi
waliopo kwani wanatosha na wala sio kweli kama polisi waliyopo hawatoshi.
Mwenyekiti
Wawamiliki wa Daladala Mkoa wa Dar es Salaam, Sabri Mabrouk, alisema adhabu
zinazotolewa kwa madereva wanaosababisha ajali ni ndogo, hivyo basi alishauri
ikitokea ajali ambayo itabainika kisheria kuwa chanzo ajali hiyo kimetokana na
uzembe dereva ni vema akahukumiwa kifo.
Hata
hivyo, Mbrouk, alisema Machi 31 mwaka huu kutakuwa na mkutano wa wamiliki wa
vyombo hivyo vya usafiri katika ukumbi wa Karimjee, mawazo yake hayo
atayawasilisha katika mkutano huo.
No comments:
Post a Comment