Sunday 5 April 2015
ASKOFU GWAJIMA: LOWASSA NI RAFIKI YANGU WA SIKU NYINGI
ASKOFU Mkuu wa Kanisa
la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amesema hakuna mtu atakayeweza atakayeweza kuvunja urafiki wake na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.
Gwajima, alisema kuwa hakumfahamu
Lowassa barabarani, kwani bali walifahamiana tangu mwaka 1996 alipokuwa Waziri wa Ardhi na
Maendeleo ya Mijini alikuwa wakishirikiana katika mambo
mengi.
Askofu Gwajima alitoa
kauli hiyo jijini Dar es Salaam leo wakati wa ibada ya Pasaka
kwenye viwanja vya Tanganyika Pakers, Kawe.
Alisema urafiki wake
na Lowassa hauwezi kuvunjika hata kama kuna maneno yanayoendelea kutolewa na
baadhi ya watu.
Askofu Gwajima, alisema kuna makundi
ya watu wanawazungumzia na kuingiza masuala ya kisiasa kwenye urafiki wao,
hata hivyo, alibainisha kama ni hivyo au sio hivyo, lakini wanapaswa kuelewa kuwa Lowassa ataendelea kuwa rafiki yake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment