WADAU mbalimbali
wa haki za binadamu wamependekeza kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali
iandae muswada wa marekebisho ya Sheria
ya kudhibiti Uchawi ambayo itasaidia kukomesha ukatili na mauaji ya watu
wenye Ualbino.
Alisema sheria
hiyo inayohitaji kufanyiwa merekebisho kuwa ni Sura ya 18 hususan Kifungu cha
8(1), kinachompa Mkuu wa Wilaya mamlaka ya kumhamisha mtu anahisiwa kuwa mchawi kwenda
kuishi sehemu nyingine.
“Idara ya
Mahakama iharakishe usikiliza wa mashauri ya mauaji na ukatili dhidi ya watu
wenye ualbino na kutoa hukumu kwa wakati ili kulinda haki za kundi
hilo,”alisema Nyanduga.
Aliongeza kuwa
kusema kuwa Jeshi la polisi kwa kushirikiana na wadau wengine, lifanye
uchunguzi na upelelezi wa kina kubaini mtandao wa wanaojihusisha na mauaji ya
watu wenye ualbino wakiwemo waganga wa jadi, wanunuzi, wakataji na watumiaji
wakuuu wa viungo vya watu hao wenye ualbino.
Aidha, wadau hao wameiomba serikali kutenga fedha za
kutosha kwa taasisi zake zinazohusika na mapambano ya kukomesha ukatili dhidi
ya watu wenye Ualbino.
No comments:
Post a Comment