MKUU wa wilaya ya Missenyi mkoani Kagera FaNkurlu,dhili amewalipia gharama za matibabu watu wote wenye ulemavu wa ngozi (albino) walioko katika wilaya hiyo, ili kuwawezesha kupata matibabu kwakipindi cha mwaka mzima kuanzia sasa.
Kadi kwa ajili
ya matibabu hayo zilikabidhiwa leo, mkuu huyo wa wilaya,wakati wa
hafla fupi ya chakula cha pamoja na watu hao wenye ulemavu wa
ngozi,iliyofanyika katika wilaya hiyo na kuwashirikisha wadau mbalimbali
wakiwamoviongozi wa dini.
Akizungumza katika hafla hiyo Nkurlu alisema
kuwa, kadi hizo walizokabidhiwawatu hao, zitawawezesha kupatiwa matibabu bila
kudaiwa kutoa malipo wao nawategemezi wao, katika vituo vya serikali vinavyotoa
huduma za afya na vile vyabinafsi vilivyosajiliwa na mfuko wa afya ya jamii (CHF).
Alisema
kuwa, mbali na
kukabidhiwa kadi hizo,
tayari
amekwishafanyamazungumzo na uongozi
wa kiwanda cha
sukari cha Kagera,
ili albino wotewatakaofika katika
kituo cha afya
kilichoko kattika kiwanda
hicho wapatiwematibabu bure, na
kuwa ombi lake limekubaliwa.
Mbali na hilo pia mkuu huyo wa wilaya ametoa
simu za mkononi kwa watu hao, ilikuwawezesha albino wasio na mawasiliano
kutumia simu hizo kutoa taarifa, pindiwanapoona watu wanaowatilia mashaka
katika maeneo yao, ili hatua za harakazichukuliwe kabla ya kutokea
madhara makubwa zaidi.
“Naendelea kufanya mawasiliano na vyama vya watu
wenye ulemavu wa ngozivya nje ya nchi, ili waweze kuwasaidia kupitia chama
chenu, kupata vitu ambavyohavipatikani huku kwa urahisi kutokana na sababu
mbalimbali ikiwamo gharamakubwa, mfano mafuta ya kuimarisha ngozi” alisema.
Aidha Nkurlu alitumia fursa hiyo kupiga marufuku
wakuu wa shule za msingi nasekondari
zilizoko katika wilaya
hiyo, kuwafukuza shule
watoto wa albino
nakuwa atakayekaidi agizo hilo atamchukulia hatua za kinidhamu.
“Kimsingi
albino ni watu ambao hawawezi kufanya kazi za kuzalisha mali kamailivyo kwa mtu
ambaye siyo albino, kwa hiyo uwezo wao
kiuchumii ni mdogo kutokana na
kutokuwa na uwezo
wa kuhimiri mikikimikiki katika shughulimbalimbali, hivyo wahahitaji
kusaidiwa,” alisema.
Akizungumza
katika hafla hiyo,
mwenyekiti wa baraza
la waislamu Tanzania(Bakwata) wa wilaya hiyo alhaji
Abubakari Rutashobya, alisema kuwa madharayote yanayowakumba albino yanatokana
na watu kuhama kwa Mungu na kwendakatika masuala ya ushirikina.
“Viongozi wenzangu wa dini mbalimbali,
tujitahidi kuwarudisha watu wetu kwaMungu, watu wafundishwe wajue kuwa Mungu ni
mgawaji kila mtu anayeingiahapa duniani ameandikiwa riziki yake, hivyo sio
busara kuua wenzetu kwa madaiya kupata utajiri” alisema alhaji Rutashobya.
Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika hivi
karibuni, wilaya ya Missenyi
inakisiwakuwa na watu wenye ulemavu wa ngozi 14.
No comments:
Post a Comment