KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday 9 June 2015

JANUARY MAKAMBA, KUCHUKUA FOMU KESHO MJINI DODOMA




MBUNGE wa Bumbuli January Makamba, anatarajiwa leo mjini Dodoma kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya wana-CCM ili aweze kuteuliwa kuwa mgombea wa nafasi ya urais katika Uchaguzi Mkuu mwaka huu.
Makamba, ambaye ni Naibu Waziri wa Wizara ya Sayansi na Teknolojia, juzi wakati akitangaza nia ya kuomba ridhaa hiyo, alisema akichaguliwa kuwa Rais hataunda Serikali ya wakwapuaji na wabinafsi.
Alisema ataunda serikali yenye utu na inayowasikiliza na kuwajali watu, inatimiza wajibu wake bila chembe ya uzembe wala ulegevu.
“Nitaunda serikali yenye Mawaziri wasiozidi 18, amabayo haitakuwa na mtu hata mmoja anayetiliwa shaka kuhusu uwezo na uwadilifu waka.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Makamba alisema baada ya kufanya tafakuri ya kina yya changamoto za sasa, akabaini kuwa nchi inahitaji uongozi wa aina mpya na ndio maama akaamua kuomba nafasi hiyo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Alisema anaomba ridhaa hiyo kwa vile anaelewa kiu ya Watanzania ya kutaka kupata uongozi mpya, wa zama za sasa, unaotoa matumaini mapya yatakayozaa Tanzania Mpya.
Makamba, alisema anaiomba nafasi hiyo akiwa anaelewa misingi iliyoijenga nchi hii ambayo ni haki, umoja, amani, mshikamano na upendo miongoni mwa Watanzania na kwamba  iko haja ya kuilinda misingi hiyo.
Aidha, alisema uongozi utakaochaguliwa mwaka huu ndio utaamua mustakabali wan chi hii, baada ya miaka 50 ya uongozi wa kizazi kilichopita, sasa ni wakati wan chi kuongozwa na viongozi wa aina mpya, wenye mtazamo mpya, fikra mpya, maarifa mapya na majawabu mapya.
“Nimesimama hapa kuwahakikishia kwamba nimefanya tafakuri ya kina na za muda mrefu kuhusu mwelekeo wa nchi yetu. Na niko tayari kutengeneza na kuongoza timu madhubuti ya Watanzania wazalendo na waadilifu watakaounda Serikali itakayojenga kesho njema,”alisema Makamba.

Makamba, alisema baada ya kuchukua fomu hiyo ataanza safari ya kwenda kusaka wadhamini maeneo mbalimbali nchini.

MWISHO

No comments:

Post a Comment