Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Kinondoni Camillus Wambura alisema tukio hilo lilitokea saa 3:00 asubuhi leo, wakati
Tanroads pamoja na Jeshi la Polisi walipokuwa katika mazungumzo ya kuweka
matuta katika barabara hiyo.
Alisema kabla
ya kuchomwa kituo hicho dereva aliyetambulika kwa jina la Yohana John aliyekuwa
akiendesha gari aina ya Coaster alisababisha ajali katika eneo hilo na kumgonga
mwanafunzi mmoja wa shule
ya Bunjua ‘A’ Radhia Omary
na kusababisha kifo chake.
Wambura, lisema
baada ya mwanafunzi huyo kupoteza maisha wanafunzi wa shule hiyo pamoja na
wananchi wa eneo hilo
walikusanyika na kulala barabarani
hali iliyosababaisha magari kutoendelea na safari zake.
Alisema
wananchi hao pamoja na wanafunzi walifunga barabara hiyo kwa muda wa saa tatu
wakidai kuwa wanataka matuta yawekwe katika eneo hilo lililopo karibu na shule hiyo ili liweze
kuwasaidia wanafunzi wakati wa kuvuka barabara.
Hali hiyo
ilileta usumbufu kwa watumiaji wa barabara hiyo kwa kufungwa na kushindwa
kuendelea na shughuli zao hali iliyosababisha polisi kutumia nguvu kuwatawanya
watu.
“Baada ya
tukio hilo polisi na Tanroads tulikaa kikao cha
dharura kilichokuwa kikielekeza utengenezwaji wa matuta ya haraka katika eneo hilo.
“Wakati
tukiendelea na mazungumzo hayo wananchi walipata mwanya wa kukivamia kituo
hicho na kukichoma moto.
“Sababu ya
wananchi hao kuchoma kituo
hicho hakuna, na wamefanya jambo ambalo si la busara na wamesahau kuwa kituo
hicho kinawasaidia watu wote wa eneo hilo,”
alisema Kamanda Wambura.
Wambura alisema
mbali na kuchoma kituo hicho pia wamechoma magari mamne ya watu binafsi
yaliyokuwa yameegeshwa pembezoni mwa
kituo hicho.
Pia alisema
wanamshikilia dereva wa Coaster aliyesababisha ajali pamoja na gari hilo.
“Kwa
sasa tupo katika zoezi la kuwasaka na kuwakamata watu wote
waliosababisha vurugu hizo ili sheria iweze kuchukua mkondo wake,” alisema
Kamanda Wambura.
Mmoja wa
mshuhuda wa tukio hilo, Moshi Sultan, alisema
kuwa tukio hilo
lilitokea saa 3:00 asubuhi baada ya gari kumgonga mwanafunzi huyo
aliyekuwa anakwenda shule.
Alisema baada
ya tukio hilo wananchi wa eneo hilo walikusanyika na kufunga barabara hali
iliyosababisha polisi kuingilia kati na kuanza mvutano kati yao na hatimaye
wananchi hao kuvamia kituo hicho na
kukichoma moto.
Alisema
wananchi hao waliwasha moto kituoni hapo pamoja na tairi za gari na kudai kuwa askari waliopo hawafanyi kazi
kwa umakini.
“Kutokuwapo kwa askari wa kutosha katika kituo hicho
kumechangia wananchi hao kuvamia kwa urahisi na kuchoma moto kituo
hicho,”alisema.
Katika tukio
jingine, moto mkubwa umezuka na kuteketeza nyumba yote inayomilikiwa na Hamisi
Katori iliyopo katika mtaa wa Mabanda Marefu Ukonga Mombasa jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Lucas Mkondya, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa
chanzo cha moto huo ni hitilafu ya umeme.
Alisema
wakati moto huo ukiendelea kuwaka alikuwepo mtoto mdogo mwenye umri wa miaka
miwili aliyetambulika kwa jina la Mohamed Shabani ambaye alikuwa amelala ndani
lakini msamaria mwema alifanikiwa kumuokoa.
Mkondya
alisema moto huo uliteketeza nyumba yote, mali na thamani zilizoteketea kwa
moto bado hazijafahamika.
Alisema
hakuna madhara kwa binadamu, moto ulizimwa na kikosi cha Zimamoto Uokoaji cha
Jiji kwa kushirikiana na wananchi wa eneo hilo.
No comments:
Post a Comment