MWENYEKITI wa Democratic Party, (DP), Mchungaji Christopher Mtikila,
anatarajia kutinga mahamani kukifungulia mashtaka Chama Cha Mapinduzi (CCM),
pamoja na amakda wake sita, akidai wameanza kampeni za Uchaguzi Mkuu mapema.
Makada hao ni Waziri Mkuu wa zamani Edward
Lowassa, na mstaafu Frederick Sumaye, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa Bernard Membe.
Wengine ni William Ngeleja, Waziri wa Chakula
na Kilimo Stephen Wasira na Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia January
Makamba, ambao wote hao waliwahi kupewa adhabu Februari 18 mwaka jana, kwa kosa
la kuanza harakati za kuwania nafasi ya
urais.
Akizungumza na wandishi wa habari
jijini Dar es Salaam jana, Mchungaji Mtikila, alisema kuwa suala la makada hao
sio la kuliacha hivi, hivi, kwani linagusa maslahi ya nchi.
Alisema, amefikia hatu hiyo baada ya
kujiridhisha kuwa wanaushahidi wa kutosha juu ya vitendo vya makada hao kwenda
kinyume na sheria za uchaguzi.
Mchungaji Mtikila, alisema makada hao
wamejiingiza kwenye vitendo vya matumizi makubwa ya fedha kwa kusafirisha watu
kwenda maeneo mbalimbali huku watu hao wakilewa na kulala bure.
“Wanasheria wetu hivi sasa wanapinda
migongo katika kukamilisha mchakato wa shauri hili n kwamba litakapokamilika
wakati wowote kuanzia sasa tutawaita kuwaeleza kwamba linakwenda mahakamani.
“Baadhi ya watu wanatafuta utawala kwa
sababu ni meno ya kumung’unya rasilimali za nchi hii,”alisema Mchungaji
Mtikila.
Mchungaji Mtikila alisema kuwa hatua
hiyo ya kukifikisha chama hicho pamoja na makada wake hazitaishia hapo bali
watafanya hivyo hata katika vyama vingine pindi watakapobaini vimeingia kwenye
vitendo vya matumizi ya fedha chafu katika upataji wa wagombea wake.
“Kumekuwa na umwagwaji kubwa wa
mabilioni ya fedha chafu kwa ajili ya kusaka madaraka jambo ni sawa na uhalifu
na uhani,”alisema Mchungaji Mtikila.
No comments:
Post a Comment