KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday 28 July 2015

NEC: ITAHAKIKISHA WAKAZI WOTE WA DAR WANAJIANDIKISHA

MWENYEKITI wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu, Damiani Lubuva, amesema baada ya kubaini changamoto zinazoikabili kazi ya uboreshaji wa daftari la mpiga kura kwa kutumia mfumo wa kieletroniki (BVR), tume inatarajia kukutana na Wakurugenzi Halmashauri za jiji la Dar es Salaam.
Jaji Lubuva, alisema hayo wakati alipozungungunza na wandishi wa habari kuhusu kazi hiyo ambayo inaendelea huku kukiwa na matatizo ambayo katika vituo vingine yamesababisha wananchi kupigana.
Alisema lengo la kukutana na wakurugenzi hao ni kufanya tathimini ili kubaini mafanikio na upungufu, kisha kutafuta ufumbuzi pale penye changamoto.
“Ingawa kuna matatizo ya machine hapa na pale bado tume yetu imeweza kufanikiwa hadi sasa katika kazi hii, ni viombe vyombo vya habari mtusaidie kufikisha taarifa sahihi baadala ya kuandika habari tofauti,”alisema Jaji Lubuva.
Jaji Lubuva, alisema katika kuwaondolea kero wakazi wa jiji la hilo NEC  imefanikiwa kuongeza mashine na kwamba hivi sasa ziko zaidi ya 6000.
Alisema kuwa NEC inajukumu la kuhakikisha kuwa hakuna mkazi wa jiji hilo anajiandikisha katika daftari hilo, akibainisha kuwa haingekuwa rahisi kusema kwamba tume itaongeza muda kwa vile muda haujaisha.
Jaji Lubuva, alitoa ufafanuzi wa uandikishaji katika wilaya za mkoa hizo kwamba katika Wilaya ya Temeke waliojiandikisha ni 188936, Ilala ni 220865 na Kinondoni ni 178961.
“Katika wilaya ya Ilala kuna kata 36 vituo 396, Temeke kata 32 vituo 572 na Kinondoni ina kata 34 vituo 706 ukiangalia utaona vijana wetu wamefanya kazi kwa uweledi pamoja na mashine hizo chache,”alisema Jaji Lubuva.
Akizungumzia, kuhusu wanafunzi kuwa huenda baadhi yao watakakosa haki yao ya kikatiba ya kupiga kura, Jaji Lubuva, aliwaonya wanasiasa kuacha kulifanya jambo hilo kuwa la kisiasa.
Naye Profesa Amon Chaligha, alitolea ufafanuzi suala hilo la wanafunzi, akisema tume inautaratibu, kwamba kila inapokaribia siku za uchaguzi hususan kuanzia Septemba, tume inatoa fursa kwa wananchi wote wakiwemo wanafunzi wanaotaka kubadilisha taarifa zao kutoka sehemu ya awali alikojiandikishia kwenda aliko.
“Naona manawazungumzia hao tu mbona hamwazungumzii wale ambao ndio kwanza wamekwenda kuanza masomo kwa mara ya kwanza kwani hawa ndio wengi kuliko hao mnaowasemea,”alisema Profesa Chaligha.
Naye Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Salum Mwalim, alisema kuwa alipata bahati ya kuzungumza na Mkurugezi Mpya wa NC, ambaye alimhakikishia kuwa atawachukulia hatua wale wote ambao utendaji una mashaka.
Alisema mkurugenzi huyo alisema kuwa atawaondoa wale wote ambao hawana ujuzi na hiyo, kwamba watatafutwa watu wenye utaalamu.
“Kwa kweli kwa muda wa siku mbili alizokaa katika ofisi hiyo ameonyesha imani kubwa kwa wadau na ndio maana kwa siku hizo kunaongezeko la watu katika uandikishaji huo,”alisema Mwalimu.
Aliwasihi wakazi wa jiji la Dar es Salaam kuacha kuogopa foleni na baadala yake wajitokeze kwa wingi katika vituo, kwa lengo la kutimiza azima yao ya kuandikishwa.

Alisema watambue kuwa bila kujiandikisha hawatapata fursa ya kupiga kura katika uchaguzi mkuu Oktoba kwaka huu.

No comments:

Post a Comment