KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Wednesday 15 July 2015

NECTA YATANGAZA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA

Mkurugenzi Mtendaji, Charles Msonde
JUMLA ya watahiniwa 38,853 sawa na asilimia 97 waliofanya mtihani wa kidato cha sita (ACSEE), Mei mwaka huu wamefaulu.
Kati ya watahiniwa hao wasichana waliofaulu ni 11, 734 sawa na asilimia 98 wakati wavulana ni 27, 119 sawa na asilimia 97.
Akizungumza na waandishi wa habari  jana mjni Zanzibar, Katibu wa Baraza la Mitihani ya Taifa (NECTA), Charlse Msonde alisema kuwa watahiniwa wa shule waliofaulu ni 34, 777 sawa na asilimia 98 huku wasichana ni 10, 576 sawa na asilimia 99 na wavulana ni 24, 201 sawa na asilimia 98.
Msonde alisema kuwa jumla ya watahiniwa 4, 076 wa kujitegemea sawa na asilimia 88 wamefaulu mtihani huo.
“Kati ya  watahiniwa 40.753  waliondikishwa kufanya mitihani ya kidato cha sita wakiwemo wasichana 12,113 (29.72%) na wavulana 28.640 (70.28%) kati ya watahiniwa waliosajiliwa na shule  walikuwa ni 35,375 na wa kujitegemea walikuwa 5,378, mwaka 2014 watahiniwa waliosajiliwa walikuwa ni 41,968 kati ya watahiniwa hao walifanya mitihani ni 39,805 sawa na 97.67 na watahiniwa 948 sawa na asilimia 2.33  hawakufanya mitihani yao” alisema Msonde.
Msonde alisema takwimu za matokeo zinaonyesha kuwa ufaulu wa watahiniwa wa shule katika masomo ya Historia, Gographia, Kingereza, Fizikia, Kemia, Balogia, Uchumi, Biashara pamoja na Akaunti umepanda ikilinganishwa na mwaka 2014.
“Ufaulu wa juu kabisa ni ule wa masomo ya Kiswahili na Historia ambapo asilimia 99 ya watahiniwa wote wa shule waliofanya masomo hayo wamefaulu, aidha ufaulu katika masomo ya Sayansi umeendelea kuimarika ikilinganishwa na ufaulu wa masomo hayo kwa mwaka jana,”alisema.
Hata hivyo Msonde alisema kuwa ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliyopata watahiniwa wa shule unaonesha kuwa jumla ya watahiniwa 31, 450 sawa na asilimia 89 wamefaulu katika madaraja ya Distinction,Merit na Credit, wakiwemo wasichana 9, 876 na wavulana 21, 574.
Aidha alieleza kuwa jumla ya watahiniwa 40, 753 waliosajiliwa kufanya mtihani huo mei mwaka huu ni watahiniwa 39, 805 tu sawa na asilimia 97 walifanya mtihani huku watahiniwa 948  sawa na asilimia 2 walishindwa kufanya mtihani huo.
Shule zilizofanya vizuri zaidi
Msonde alisema kuwa ubora wa shule umepangwa kwa kutumia kigezo cha wastani wa pointi na upangaji wa shule hizo umezingatia shule zenye idadi ya watahiniwa wasiopungua 30.
Alisema shule kumi bora ni Feza Boy’s (Dar es Salaam), Runzewe (Geita), Feza Girl’s (Dar es Salaam), Sumbawanga (Rukwa), Ivumwe (Geita), St Mary’s Mazinge juu (Tanga), Vwawa (Mbeya), Kisimiri (Arusha), Namabengo (Ruvuma) pamoja na Scolastica (Kilimanjaro).
Shule kumi  za mwisho
Alisema kuwa shule kumi za mwisho ni Bariadi (Simiyu), Ilongero (Singida), Lwangwa (Mbeya), Kilangalanga (Pwani), Kaliua (Tabora), Logoba (Pwani), Iwalanje (Mbeya), Mtwara Technical (Mtwara), Kwiro (Morogoro) pamoja na Meta (Mbeya).
Watahiniwa waliofanya vizuri zaidi
Msonde alisema kuwa watahiniwa waliofanya vizuri zaidi wamepatikana kwa kulinaganisha wastani wa pointi (GPA) kwenye masomo ya tahasusi (Combination) pamoja na wastani wa alama za jumla walizopata.
Alisema kuwa watahiniwa hao ni Ramadhani Gembe (Feza Boy’s), Lesian Lengare (Ilboru), Hunayza Mohamed (Feza Girl’s), Rosemary Chengula (St Mary’s Mazinde juu), Kevin Rutahoile (St Joseph’s Cathedral), Anderton Masanja (St Joseph’s Cathedral), Joseph Pasian (Iliboru), Lupyanal Kinyamagoha (Mzumbe), Yonazi Senkondo (Feza boy’s) pamoja na Meghna Solanki (Shaaban Robert).
Msonde alisema kuwa tathimini ya awali ya matokeo kwa watahiniwa wa shule yamezidi kuimarika kwani ufaulu umepanda kwa asilimia 0.61 kutoka asilimia 98.26 mwaka 2014 hadi asilimia 98.87 kwa mwaka huu.
Alisema tathmini ya ufaulu wa shule mbalimbali inaonesha kuwa katika shule kumi bora kitaifa shule za serikali ziko tano na zisizo za serikali ziko tano, aidha alieleza katika shule ishirini bora kitaifa shule za serikali ziko 13 na zisizo za serikali ni saba.
Alisema kuwa kuhimarika huko kwa ufaulu kwa mwaka huu ikilinganishwa na mwaka jana ni matokeo ya juhudi zinazoendelea kufanywa na serikali katika kuboresha elimu nchini.
Matokeo yaliyozuiliwa 
Alisema kuwa watahiniwa 10 wa shule ambao waliugua wakati wa mtihani na kushindwa kufanya mitihani kwa baadhi ya masomo matokeo yao yamezuiliwa.
“Watahiniwa hawa 10 na wengine 25 ambao awakufanya masomo yote wamepewa fursa ya kufanya mitihani yao Mei, 2016,” alisema.
Matokeo ya mtihani yaliyofutwa
Msonde alisema kuwa baraza limefuta matokeo yote ya watahiniwa watano waliobainika kufanya udanganyifu.
Aidha Msonde alisema anazipongeza kamati za uendeshaji mitihani za mikoa na wilaya, wakuu wa shule na wasimamizi kwa kuzingatia na kusimamia ipasavyo taratibu za uendeshaji wa mithani hiyo.
“Nwapongeza sana imeweza kuzuia kwa kiasi kikubwa udanganyifu lakini pia nawapongeza watahiniwa wote waliofanya vizuri na kutojihusisha na udanganyifu,” alisema.
Matokeo mengine yaliyotangazwa
Matokeo mengine ya mitihani yaliyotangazwa na  katibu huyo ni Ualimu daraja la A, mtihani wa Stashahada ya ualimu Sekondari, stashahada ya ualimu ufundi na ualimu daraja A kozi maalum.
Watahiniwa walisajili kufanya mtihani daraja la A ni 14,106 sawa na asilimi 62 .81ya watahiniwa wote waliosajiliwa watahiniwa wa mtihani wa ualimu ndaraja A kozi maalum 158  sawa na asilimia 53.80 ya watahiniwa wote waliosajiliwa kati ya waliosajiliwa 155 walifanya mitihani huku watatu wakiwa hawakufanya mitihani hiyo.
Watahiniwa waliosajiliwa kufanya stashahada ya ualimu wa Sekondari ni 4,788 kati ya walisajiliwa 4,765 walifanya mitihani yao watahiniwa 23 hawakufanya mitihani ,katika watahiniwa wa stashahada ya ufundi waliosajiliwa walikuwa ni 4  watahiniwa watatu walifanya mtihani na mmoja hakufanya .




No comments:

Post a Comment