KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday 31 July 2015

VYAMA VYA SIASA VYATAKIWA KUYAJENGEA UWEZO MAKUNDI MAALUMU

Dk. Ave-Maria Semakafu
VYAMA vya Siasa nchini vimetakiwa kuyajengea uwezo makundi ya watia nia wa wanawake, watu wenye ulemavu na vijana ili yaweze kushiriki katika mchakato wa chaguzi mbalimbali nchini.
Hayo yalisemwa jijini Dar es Salaam jana, Mratibu wa Mtandao wa Jinsia (TGNP Mtandao), Grace Kisetu, wakati alipokuwa akitoa mrejesho kwa viongozi wa vyama hivyo, uliyotokana na mafunzo kwa watia nia hao yaliyofanyika hivi karibuni.
Alisema, hivyo kwa vile watia nia hao, wakati wa mafunzo  walieleza kwamba kila kinapofika kipindi cha uchaguzi makundi hayo yamekuwa yakikabiliwa na matatizo ikiwemo rushwa, upendeleo wa kidugu bila kujali uwezo wa wahusika.
“Mafunzo haya yanalenga kuwajengea uwezo makundi  haya ili yaweze kuteuliwa ili wapate haki katika vyama vyao, hatimae waweze kuingia katika uchaguzi,”alisema Grace.
Alisema, walianza kutoa mafunzo kwa wadau na jamii kwa ujumla ili na yenyewe ione kuwa mwanamke akipewa uongozi anawaweza hivyo aminike.
Hata hivyo mafanikio ya mafunzo hayo mafanikio yake yataanza kuonekana katika uchaguzi utakaofanyika mwaka 2020.
Naye Mratibu wa Ulingo, Dk. Ave-Maria Semakafu, alisema kuwa kumekuwa na matatizo ya kuwapata watia nia wakati wa mafunzo kutoka katika vyama hivyo.
Alisema, hali hiyo imekuwa ikichangiwa vyama vyote vya siasa nchini kutokuwa na mawasiliano kutoka ngazi ya chini hadi taifa.
Dk. Semakafu, alisema kutokana na mazingira hayo aliwataka viongozi wa vyama hivyo kuanzisha daftari la kudumu la wanachama.
“Kumekuwa na ubabaishaji wakati wa kuwakuwakilisha majina ya washiriki wa mafunzo kwani baadhi ya viongozi wamekuwa wakipeleka majina ya ndugu zao au kuuza nafasi hizo, sasa hii inatia shaka,”alisema Dk. Semakafu.

Alisema kwa chama ambacho kina lengo la kuongoza nchi  kuanza kujiingiza katika vitendo vya rushwa hiyo ni hatari na kwamba hakiwezi kuaminika tena katika jamii.

No comments:

Post a Comment