Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damiani Lubuva |
Hata hivyo kwa ipande wa Jimbo jipya la Mbagala, lililoko
katika Halmashauri ya Temeke wakazi wake pamoja na viongozi wamekuwa wagumu
kuzungumzia hilo.
Akizungumza na wandishi jijini jana, kwaniaba ya wenzake,
Ephraim Kinyafu, ambaye ni diwani anayemaliza muda wake, alisema wananchi
hawana shida na ngawanyo huo bali hawa kuridhi na hatua za serikali kulifanya
Jimbo la Ubungo kuwa Wilaya bali walitaka liwe Halimashauri.
Alisema, kuridhika kwao huko kunatokana na NEC kupokea
maombi na mapendekezo ya kuanzisha jimbo la jingine la uchaguzi kutoka kwa wadau
wa lillilokuwa Jimbo la Ubungo.
Aidha, alizitaja kata zilizoko katika Jimbo hilo kuwa ni Saranga, Goba, Mbezi, Kwembe, Msigani na Kibamba yenyewe. “Ingawa wenzetu hawa wameligawa jimbo hili kwa dhamira mbaya inayolenga uchaguzi, ni wahakikishie kuwa tutashinda majimbo yote kwa maana ya Jimbo la Ubungo na lile jipya la Kibamba,”alisema Kinyafu.
Aidha, alizitaja kata zilizoko katika Jimbo hilo kuwa ni Saranga, Goba, Mbezi, Kwembe, Msigani na Kibamba yenyewe. “Ingawa wenzetu hawa wameligawa jimbo hili kwa dhamira mbaya inayolenga uchaguzi, ni wahakikishie kuwa tutashinda majimbo yote kwa maana ya Jimbo la Ubungo na lile jipya la Kibamba,”alisema Kinyafu.
Alisema, kugawanywa kwa jimbo hilo kutasaidia kuchechemua
maendeleo ya kijamii katika jimbo jipya la Kibamba, kwa mfano, itabidi katika
jimbolo jipya kujengwe hospitali kama ilivyo katika makimbo mapya.
Kwa upandea wa Jimbo la Mbagala mmoja wa viongozi ambaye
hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema hadi sasa hawajui ni kata zipi
zimekwenda kigamboni au nizipi zimechukuliwa kutoka Temeke.
Alisema, ingawa kuna taarifa kuwa mpaka ni wa jimbo la
Mbagala na Kigamboni ni barabara kubwa, hata hivyo, anajiuliza kama ni hivyo
jimbo hilo litakuwa dogo kwa sababu haamini kama Temeke itakubali kumegwa eneo
lake.
Hata hivyo, kiongozi huyo, alisema kwa vile hawajaiona
taarifa hiyo ya NEC, itawabidi wasubiri kuona mgawanyo wa kata hizo.
Jitiahada za wandishi ili kumpata Ofisa Habari wa Halmashauri hiyo ziligonga
mwamba baada ya simu yake kuita muda mrefu bila kupokelewa.
Juzi Tume hiyo ya uchaguzi ilitangaza majimbo orodha ya
majimbo mapya 26 ya uchaguzi Tanzania Bara kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu
unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka Huu.
No comments:
Post a Comment