Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi |
MKUU wa Wilaya ya Ilala Raymond Mushi akishirikiana na Mkurugenzi wa
Manispaa hiyo Issaya Mngurumi, wametoa siku mbili kwa wafanyabiashara
ndogondogo (Wamachinga), waliovamia eneo la Jangwani kuwa hadi Jaulai 30 wawe
wameondoka.
Kauli hiyo inakuja siku moja baada ya Baraza la Taifa la Hifadhi na
Usimamizi wa Mazingira (NEMC), kuutaka uongozi wa Manispaa ya Ilala kusitisha zoezi
la ugawaji wa eneo la Jangwani kwa wafanyabiashara ndogo ndogo (machinga) kwa
kuwa eneo hilo si salama.
Akizungumza na wandishi jijini Dar es Salaam jana, Mushi, alisema
kuwa Manispa hiyo haijagawa eneo hilo kama inavyodaiwa wafanyabiashara hao.
Alisema, wamefikia hatua hiyo baada ya kubaini kuwa eneo hilo
limevamiwa na watu ambao hawakuwa lengo la manispaa hiyo kwani waliyotakiwa
kwenda pale walikuwa ni wamachinga wanaotandika biashara zao chini katika eneo
la Kariakoo.
Mushi, alisema baada ya siku mbili hizo kupita manispaa hiyo itatumia
nguvu kuwaondoa katika eneo hilo tena bila kujali gharama walizoingia katika
ujenzi huo.
“Ni vema wakazitumia siku hizi mbili kuboa mabanda yao ili kuepuka
hasara ambayo inaweza kujitokeza baada ya muda uliyotolewa kupita,”alisema
Mushi.
Mushi, ambaye baadhi ya wafanyabishara hao walidai kuwa alikuwa ni
mmoja wa viongozi alitoa agizo la wao kwenda katika eneo hilo, alipinga vikali
kuhusika katika mpango huo.
“Mimi sina maeneo mwenye maeneo ni Halmashauri ya Ilala kwa hiyo
siana uwezo wa kugawa maeneo kama wanavyodai,”alisema Mushi.
Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Mngurumi, aliwataka wafanyabiashara hao
kutekeleza agizo haraka kabla muda haujapita kinyume chake atapeleka greda kwa
ajili ya kuvunja mabanda yote.
“Kumetokea upotoshaji kwani wakati wanawapeleka wafanyabiashara hao
wa Kariakoo tuliwaeleza wazi kuwa hawana ruhusa ya kujenga mabanda bali
walikubaliana kuwa wataendesha biashara zao kwa kuzitandika chini,”alisema
Mngurumi.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini juzi, Mwanasheria wa Baraza
hilo, Manchare Suguta, alisema, wakiwa wasimamizi wa mazingira wamelazimika
kuwaandikia uongozi wa manispa hiyo barua Julai 24 mwaka huu wakiwataka
kusitisha uamuzi wao haraka.
No comments:
Post a Comment