KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Thursday 20 August 2015

NCCR-MAGEUZI YAPATA MAJIMBO 19 KATIKA MGAWO WA MAJIMBO 265

CHAMA cha NCCR-Mageuzi kimepata majimbo 19 baada ya kukamilika majadiliano ya ugawaji wa majimbo kwa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Chama hicho kimepata majimbo hayo kati ya 265 ndani ya vyama vinavyounda Ukawa ambavyo ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Chama cha Wananchi (CUF), NLD na NCCR-Mageuzi.
Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Nderakindo Kessy .
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mkuu wa Uchaguzi, Mwalimu Nderakio Kessy, alisema majimbo hayo yamefikia 19 baada ya kukamilika majadiliano kuhusu majimbo 12 yaliyokuwa yamebaki kati ya 265.
“Kama mnavyofahamu kwamba awali chama chetu katika mgawanyo kilipata majimbo 14, lakini hivi sasa majimbo yetu yameongezeka kufikia hadi 19,”alisema  
Aliyataja majimbo hayo ni Kasulu Vijijini na Mjini, Buyungu, Muhambwe, Kigoma Kusini, Manyovu, Mwanga, Vunjo, Mtwara Mjini, Mufundi Kusini.
Mengine ni Gairo, Kibakwe, Mpwapwa, Mtera, Ngara, Mbinga Vijijini, Ileje, Nkenge na Serengeti.
“Tumekubaliana kati ya majimbo 265 ya uchaguzi NCCR-Mageuzi inasimamisha wagombea katika majimbo 19 kati ya majimbo hayo 265,”alisemaMwalimu Nderakio.
Hata hivyo, Mwalimu Nderakio, alishindwa kuyataja majina ya wagombea na majimbo yao kutkana na mchakato wa kukamilisha ujazaji wa fumu kutokamilika kwa asilimia 100.
Alisema hadi sasa mchakato huo umekamilika kwa asilimia 86, huku kwa wale ambao bado kukamilisha wanaendelea ili waweze kukamilisha na kutangazwa majina hayo.
Aidha, alikanusha taarifa zilizochapichwa kwenye chombo kimoja cha habari kuhusu kujitoa kwa chama hicho katika Ukawa na kusema kwamba hazina ukweli wowote.
“Chama kina utaratibu wake kila kinapotaka kutoa taarif inafahamika kuwa msemaji ni mwenyekiti, kwa aliyetoa taarifa hiyo chama kimebaini kuwa aliyetoa hayuko Dar es Salaam,”alisema  
Mwalimu Nderakio, alisema, msimamo wa chama hicho ni kutokujitoa katika Ukawa na kuongeza kuwa kitakuwa cha mwisho kutoka.
Alisema lengo kuu la kuanzishwa umoja huo ulitokana na yale yaliyokuwa yakiendelea ndani ya Bunge la Katiba jambo ambalo kwa zaidi ya miaka 20 chama hicho kilikuwa kikipigania kupatikana Katiba Mpya kwa ajili ya ustawi wa 

No comments:

Post a Comment