KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Thursday 28 January 2016

VIONGOZI WA DINI WATOA MAONI KUHUSU TBC1


Sheikh wa Jumuiya, Taasisi za Kiislam na Shura za Maimamu, Rajab Katimba

BAADHI ya viongozi wa dini nchini wamelitaka Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), kuacha kuzuia wananchi katika kufuatilia wa wakilishi wao bungeni kwani kunawanyima hivyo ni sawa na kuwanyima haki ya kupata habari. Sheikh wa Jumuiya, Taasisi za Kiislam na Shura za Maimamu, Rajab Katimb, alisema Jumuiya hiyo imesikitishwa na Kitendo hicho kwani kinakwenda kinyume na mfumo wa kujenga demokrasia kwa kutumia vyombo vya habari.
Alisemam kuwa TBC halipaswi kuendeshwa kisiasa tena kwa kudhani kuwa lipo kwa ajili ya Chama tawala baadala ya wananchi ambao ndiyo wenye shirika hilo.
“Wanachofanya TBC pamoja na serikali yake hakikubaliki na hakieleweki na kikubwa zaidi wanachofanya ni sawa na kufanya sensa ya taarifa kisha watowe wanachotaka.
“Kama kweli wamezuia bunge kwa madai ya uchochezi hiyo siyo kweli kwani kama nivitendo vya uchochezi basi kwa kiasi kikubwa chama tawala kimehusika kwa kiasi kikubwa mfano ni Zanzibar wakati wa sherehe za Mapinduzi baadhi ya wafuasi walipita mbele ya viongozi yaliyokuwa na maneno ya kibaguzi ambayo yanaleta uchochezi,”alisema Sheikh Katimba.
Sheikh Katimba, alisema hakuna haja kwa vyombo vya habari kudhibitiwa kwa vile vyombo hivyo hivi sasa vinachikua nafasi kubwa katika kukomaza demokrasia kwa hiyo serikali haina haja ya kuwanyima watanzana uhuru wakupata taarifa.
Alisema kuna haja kwa serikali kutoa uhuru kwa vyombo vya habari ili viweze kuwahabarisha wananchi baadala ya kuvikatisha tama vyombo hivyo mfano mzuri ni kufutwa kwa gazeti la MAWIO.
Naye Askofu wa Kanisa la Kipentekosti William Mwamalanga, umoja wao unalaani kitendo kilichofanywa na wizara husika kwani kimeonyesha wazi kutojali haki ya wananchi ya kupata habari.
Alisema TBC ni shirika la Watanzania ambalo kwa kiasi kikubwa bdiyo sikio lao la kuwafikishia taarifa mbalimbali hususan zinazotokea hivi sasa bungeni.
Akofu Mwamalanga, alisema kuwa kama TBC imeshindwa kutoa huduma ni vema likatoa haki hiyo, kwa vyombo vingine vya habari kupewa nafasi ya kuwafikishia wananchi habari hizo za Bunge ambazo ni muhimu sana kwa wananchi.
“Shirika hili ni letu sote tena linaendeshwa kwa kodi za Watanzania kwa hiyo kitendo cha kuzuia taarifa ni sawa na kuwafanyia dhuluma walipa kodi wake,”alisema Mwamalanga.
Kwa upande wake James Watondoha, ambaye ni mkazi wa Mbezi, alisema pamoja na kusikitishwa na kitendo cha kuzuiwa taarifa hizo za kibunge lakini bado hakuridhishwa na mwanzo wa Bunge hilo.
Alisema, kuwa alitarajia kuwaona wabunge hao wakijikita zaidi katika kupigania matatizo ya wananchi baadala yake wabunge hao walijikita zaidi kwenye kutunishiana misuri jambo ambalo halitawasaidia Watanzania.
Watondoha, alisema kuwa kama wabunge hawataacha itikadi za vyama vyao katika kujadili shida za wananchi kuna hatari Bunge hilo likamalizika bila ya mijadala yeote kutopatiwa ufumbuzi.

No comments:

Post a Comment