KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Wednesday 27 April 2016

MAVUNDE AWAONYA WAAJIRI WASIYOFUATA SHERIA ZA KAZI


NAIBU WAZIRI, ANTHON MAVUNDE

NAIBU Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na walemavu mheshimiwa Anthony Mavunde, amesema baadhi ya waajiri ambao hawataki kutoa mikataba kwa mujibu wa sheria za kazi kiama chao kimekaribia.
Aliyasema hayo baada ya kubaini ukiukwaji wa sheria za kazi katika kampuni mbalimbali za watu binafsi kumekuwa chanzo cha misuguano kati ya waajiri na wafanyakazi sehemu za kazi.
Akizungumza kwenye kipindi cha Dakika 45; kinachorushwa na ITV kila Jumatatu kuanzia saa 3 usiku, Mavunde, alisema serikali imechoshwa na misuguano hiyo inayotokana na waajiri kupuuza madai ya wafanyakazi wao wanaodai mkataba wa ajira.
Alisema, ili kuwabana waajiri hao, wasiyopenda kufuata sheria za kazi serikali imeamua kuziangalia upya sheria hizo, kwa ajiri ya kuzifanyia marekebisho ambayo yataweza kutoa adhabu kali ya papo kwa papo kwa mwaajiri yeyote ambaye atakaidi kutoa mkataba kwa mfanyakazi.
“Niliwahi kufanya ziara za uguzi katika kampuni anbazo siwezi kuzitaja kwa kweli nilibaini kuwepo kwa mambo ambayo ni kinyume na sheria za kazi  na yanafanyika kwa vile mhusikaanajua anaweza kupigwa faini kisha akaendeleanautaratibu huohuo mbovu,”alisema Mavunde.
Alisema, anaamini kuwa utaratibu huo wa adhabu kali unaweza kuwa suluhisho ukilinganisha na huu wa sasa wa kufikishana kufunguliana kesi kwenye mahaka ya kazi.
Mavunde, alisema licha ya mpango kuandaliwa lakini bado  Wizara  yake inawataka waajiri wote kuwapa wafanyakazi wao mikataba na kuwaruhusu kujiunga na mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na kuruhusu kufunguliwa matawi ya vyama vya wafanyakazi katika ofisi zao.
“Unajua kitendo cha kuwanyima mkataba wafanyakazi kuna wanyima haki ya kuwekewa akiba katika mifuko hiyo ya kijamii pia wanaikosesha serikali kodi sasa tunawataka wabadilike kwani siyo kila kitu lazima waelekezwe na serikali kwani mbona sheria za kazi ziko wazi,”alisema Mavunde.
Mavunde, alisema nia yake kubwa ni  kuona Sheria ya Kazi inafuatwa na waajiri wote ili kujenga Tanzania ambayo itakuwa haina misuguano baina ya wafanyakazi na waajiri jambo ambalo litasaidia kuleta maendeleo kwa kasi iliyoanzishwa na Serikali ya Awamu ya Tano.

No comments:

Post a Comment