KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Saturday 28 May 2016

CHAKUA: TEMESA PUNGUZENI TOZO YA KUVUSHA DALADALA KATIKA DARAJA LA KIGAMBONI


MWENYEKITI WA CHAKUA, HASSAN MCHANJAMA (KUSHOTO), AKIWA NA OFISA WAKE, GERVAS RUTAGUZINDA

CHAMA cha Kutetea Abiria (Chakua), kinatarajia kukutana na Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), ili kujadili tozo ya sh. 7000 ya kuvusha magari ya kusafirisha abiria (daladala), katika daraja la Kigamboni ambayo ina lalamikiwa na wamiliki wa vyombo hivyo kuwa ni kubwa.
Mwenyekiti wa Chakua, Hassan Mchanjama, aliyasema hayo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wa miliki wa daladala hizo, kudai kwamba wameshindwa kulipa tozo hiyo, hivi sasa baadhi yao wamesitisha huduma kwa vile wamekuwa wakipata hasara kila waanapovusha magari yao.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Mchanjama, alisema lengo la kukutana na Temesa wiki ijayo ni kutaka kuona wamiliki hao wanasikilizwa lakini kubwa ni kutetea ambiria wao.
Alisema, wamefikia hatua hiyo baada ya kusikia kuwa baadhi ya wamiliki wa daladala hizo kusitisha huduma katika ruti hiyo, kwa kuogopa tozo hiyo kwa kila safari, hali ambayo imesababisha kukosekana kwa usafiri kwa wakazi wa Kigamboni.
“Chakuwa imepokea malalamiko kutoka kwa abiria pamoja na wamiliki wa daladala kuwa daladala zao zinatozwa ushuru wa sh.7000 kwa kila safari moja kwa siku karibu sh. 150,000  huku wakipata hasara kutokana na hali hiyo wamiliki wameacha kupeleka magari na kufanya abiria wahangaike kwa kukosa usafiri.
“Tunatambua juhudi za serikali ni kuwapunguzia adha ya usafiri wananchi wake, lakini kutokana na malalamiko hayo ya abiria yanaondoa matumaini yao ya kuondokana na adha hiyo ya usafiri kwani hivi sasa baadhi wameanza kusafiri na vyombo vya majini ambavyo usalama wake ni mdogo hivyo kuhatarisha maisha ya abiria hao,”alisema Mchanjama.
Mchanjama, alisema Chakua wanatarajia kuishauri Temesa kuangalia tozo hiyo upya kwa lengo la kuifanyia marekebisho ili wamiliki hao waweze kutoa huduma kwa abiria wao ambao hivi sasa wanataabika.

No comments:

Post a Comment