KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Saturday 28 May 2016

MARWA: SPIKA WATAJE WANAOINGIA BUNGENI WAKIWA WAMETUMIA KILEVI



SPIKA wa Bunge Job Ndugai ametakiwa kuweka hadharani majina ya wabunge, aliyodai kuwa wamekuwa wakiingia bungeni huku wakiwa wametumia kilevi.
Kauli hiyo inakuja siku chache baada ya Rais John Magufuli kutengua uteuzi wa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, anayedaiwa kuwa alionekana amelewa muda wa kazi pale alipokuwa akijibu maswali ya wabunge katika kipindi cha maswali na majibu bungeni.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam, jana Mwenyekiti wa Jukwaa la Watetezi wa Rasilimali wasiokuwa na Mipaka (WARAMI), John Marwa, alisema wanampongeza Rais kwa hatua aliyochukuwa dhidi ya waziri huyo kwa vile itakuwa fundisho kwenye jamii iliyozoea kuishi maisha ya mazoea.
Alisema wamefikia hatua hiyo, kutokana na kiongozi huyo wa Bunge kukiri akiwa bungeni kwamba kuna wabunge wanakuwa wa,elewa hata kuvuta bangi wakati wa mikutano ya Bunge ikiendelea hali iliyowafanya wananchi kupoteza imani na chombo hicho muhimu.
“Kwa sababu Bunge ni chombo ambacho kinasemea wananchi dhidi ya Serikali na kama kiongozi wa Bunge amekiri jambo hili tunamtaka aweke wazi majina ya hao Wabunge hadharani ili chombo hicho cha uwakilishi kirudishe heshima yake kwa Umma.
“Pia tunaomba sheria kali zitungwe ili kukidhi na kutoa adhabu kali kwa Wabunge watakaobainika kujihusisha vitendo hivyo vya aibu wa wapo ndani Bunge,”alisema Marwa.
Aidh, Marwa alisema endapo kiongozi huyo atashindwa kutaja majina ya wabunge hao, basi watamtaka awaombe radhi wabunge na Watanzania ili waendelee kuwa na imani na wabunge wao.
“Hatuwezi kusema tutamchukulia hatua gani endapo atashindwa kufanya hivyo,  cha msingi hapa ni suala la tunasubiri muda,”alisema Marwa.
Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa Jukwaa la Watetezi wa Rasilimali wasiokuwa na Mipaka WARAMI, Evance Kamenge, alimelitaka Jeshi la Polisi Kitengo cha Usalama Barabarani (Trafic), kupitia upya sheria ya barabara za Mabasi ya endayo haraka, ikiwa ni pamoja na kutambua kuwa yale ni magari na siyo treni.
“Waifahamishe Kampuni ya UDRT kwamba, lazima waajiri madereva wenye sifa za kuendesha magari ya abiria, pili  madereva watambue kuwa wanaendesha magari siyo treni.
“Kwa kuwa huu ni usafiri mpya WARAMI tunapendakeza Mwekezaji wa mradi huu ahakikishe anatoa ajira kwa madereva wenye sifa stahiki na wanaojua vema sheria za barabarani  kwani tumebaini wapo baadhi ya madereva ambao wamejenga kiburi kwa kuitumia vibaya sheria ya mbasi hay,”alisema Kamenge.
Aidha, Kamenge, WARAMI, inamtaka mwekezaji kuangalia uimarishaji wa vitoa ishara au honi kwa mabasi yake upya kwani hadi sasa havijakuwa msaada wa kuepusha ajali katika makutano ya barabara.
Alisema tangu kuanza mradi huo takribani wiki mbili sasa tayari kuna kumeripotiwa vifo vya watu watano waliyofariki kwa ajali zilizotokana na uzembe wa madereva wa mabasi hayo au watumiaji wa barabara hizo.
Kamenge, alisema wakati mwingene watumiaji wa barabara hizo, wamekumbwa na ajali hizo kutokana na kutoelewa matumizi ya barabara hizo kwani baadhi yao wamekuwa wakiingia kwenye njia hizo hali inayosababisha wagongwe.
Pia, alisema WARAMI inapendekeza Kamati ya Usafirishaji pamoja na Mkuu wa Mkoa kukaa chini upya kutafakari matumizi ya barabara hiyo hususan kwa wavukao kwa miguu.


No comments:

Post a Comment