KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Saturday 28 May 2016

PROFESA MBARAWA AWATAKA MAKANDARASI NCHINI KUUNGANA.

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa, amesema Serikali itaweka mazingira wezeshi ili kuwawezesha Makandarasi wazawa kupata miradi mingi ya ujenzi wa miundombinuya nchini.
Akifunga mkutano wa siku mbili wa Makandarasi Prof. Mbarawa amesema, Serikali itatenga miradi mikubwa maalum kwa ajili ya Makandarasi wazawa ili kuwajengea uwezo.
“Kazi yenu ni moja tu ni kuwajengea watanzania miundombinu iliyobora ili wa/kie uchumi wa kati i/kapo 2025”, amesema Prof. Mbarawa.
Amesisitiza umuhimu wa Makandarasi wazawa kuungana ili waweze kupata miradi mingi ya Serikali na kuijenga kwa muda sahihi kwa thamani inayowiana na fedha wanazolipwa.
Amezitaka Taaasisi za fedha nchini zipunguze riba za mikopo kwa Makandarasi wazawa ili kuwawezesha kukua na hivyo kupata miradi mingi ya ujenzi ndani na nje ya nchi.
“Changamkieni fursa katika ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Tanga-Tanzania hadi Hoima- Uganda (km 1410), ujenzi wa reli ya kati na ujenzi wa viwanda vikubwa vya kati na vidogo”,amesisitiza Prof. Mbarawa.
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (Sekta ya Ujenzi), Mhandisi Joseph Nyamhamga, amewataka Makandarasi kujipanga vizuri kutumia fursa zilizopo katika bajeti ijayo kwa kujenga miradi kwa ubora na gharama sahihi.
Amewaonya Makandarasi kuacha kufanya kazi chini ya kiwango na kujiepusha na vitendo vya rushwa kwani husababisha miradi kutokuwa na ubora uliokusudiwa.
Naye, Mwenyekiti wa Bodi ya Makandarasi Mhandisi Consolata Ngimbwa amemhakikishia Waziri Prof. Mbarawa kuwa Makandarasi wazawa wataungana katika kutekeleza miradi mikubwa na kuiomba Serikali watengeneze mazingira ya Makandarasi wazawa kushirikiana na Makandarasi wa nje katika ujenzi wa miradi mikubwa.
Asilimia 46 ya Bajeti ya Maendeleo ya mwaka 2016/2017 imetengwa kwa ajili ya ujenzi wa miradi mbalimbali ya miundombinu hapa nchini.

No comments:

Post a Comment