KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Monday 16 May 2016

WATU 11 WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA TUHUMA ZA UBAKAJI NA UZALILISHAJI-MOROGORO


MKUU WA JESHI LA POLISI NCHINI (IGP), ERNEST MANGU

WATU 11 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Morogoro wakidaiwa kumbaka binti wa miaka 21(jina linahifadhiwa).
Wakati huo huo, Mtandao wa Jinsia (TGN), unavitaka vvyombo vya dola kuchukuwa hatua za haraka kuhakikisha watuhumiwa hao kesi yao inaendeshwa kikamimilifu naa uminifu ili haki itendeke na iwe findisho kwa watu wenye tabia kama hizo.
Akizungumza na wandishi kwa njia ya simu jana, Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Urlich Matei, alisema tukio hilo limetokea Aprili 28 mwaka huu kwenye nyumba ya kulala wawageni itwayo Titii iliyoko Dakawa wilayani Mvomero.
“Chanzo cha tukio hilo ni kwamba binti huyo alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Thabit,”alisema Matei.
Alisema alikumbwa na binti huyo alikumbwa ba mkasa huo baada alipigiwa simu na Zuber Thabit (30) mkazi wa Mbarali Mbeya, akimtaka aende katika nyumba hiyo ya kulala wageni, hata hivyo wakiwa chumbani aliingia Iddy (32) Adamu mkazi wa Makambako, huku akiwa na kisu mkononi.
“Adamu alimtaka binti huyo asipige kelele na kumtaka afanye kila atakachomuelekeza ndipo alipo walipotekeleza ukatili huo na kumtisha kuwa asitoe siri hiyo vinginevyo atauawa,”alisema Kamanda Matei.
Alisema wakati Iddy akimtisha kwa kisu Thabit  ambaye kazi yake ni dereva aliendelea kumbaka na kumdhalilisha binti huyo.
“Wakati Thabit akiendelea Iddy alikuwa akiendelea kurikodi picha za video kupitia simu yake kisha baadae kuzituma picha hizo kwenye simu kwa njia ya Whatsapp kwa mtu aitwaye Rajabu Salehe (26), mkazi wa Dakawa,”alisema.
Matei, alisema baada ya Salehe kuzipokea naye alizisambaza kwa picha hizo katika mitandao mbalimbali.

Aidha, Kamanda Matei, alisema baada ya tukio hilo la kikatili kuripotiwa Kituo cha Polisi Dakawa Mei 4 mwaka huu, uchunguzi ulianza mara moja, kisha kufanukiwa kukamata watuhumiwa hao 11 wakiwemo wabakaji hao na waliyozisambaza tisa kati ya hoa 11.
Aliwataja watuhumiwa hao wengine tisa kuwa ni Rajabu Salehe (26), Said Othman ((26), Musini Ngai (36), Said Mohamed (24), John Peter (24),.
Wengene ni Hassan Ramadhan (27), Ramadhan Ally (26) na Lulu Peter (38), Magreth Njonjo (30), wote wakazi wa Dakawa.
Kamanda Matei, alisema watuhumiwa hao wamefunguliwa kosa la kusambaza picha za utupu chini ya kifungu cha 14 (1) (a) cha Sheria ya Makosa ya Mtandao.
Aliongeza kwa kusema kuwa jitihada za kuwatafuta watuhumiwa wengine zinaendelea.
Aidha, jeshi la polisi mkoani humo linatoa onyo kwa wananchi wote kuwa makini na matumizi ya mitandao ya kijamii kwa kutoshiriki makosa kwani sheria ipo na inafanyakazi ipasavyo.
Mkurugezi Mtendaji wa TGNP, Lilian Liundi, alisema,wanalaani tukio hilo la ukatili wa kijinsia kwani kitendeka ni udhalilishaji mkubwa na unyama.
Alisema unyama aliyofanyiwa mwanamke huyo, ni kinyume na sheria maalum ya makosa ya kujiamihiana (SOPA) ya mwaka 1998.
 “Tunataka Watanzania kuacha mara moja kusambaza video au picha za udhalilishaji wa wanawake, watoto, wazee au makundi yiyote ambazo zinaonesha faragha au kuwadhalilisha kwa namna yeyote kwani ni kinyume na sheria na Katiba ya nchi,”alisema Lilian.
Lilian, alisema serikali imeridhia mikataba na matamko  mengi kuhusu haki za wanawake na usawa wa kijinsia mfano mkataba wa kutokomeza aina zote za ukatili na dhuluma dhidi ya wanawake na watoto (CEDAW) pamoja Mkataba wa haki za watoto (CRC).
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Ummy Mwalimu baada ya kuiona kwenye mitandao video hiyo, alikemea kwa mhuvu na kusema huo ni udhalilishaji wa hali ya juu na hauvumiliki.
“Nakemea kwa nguvu zangu zote waliofanya kitendo hiki. Ni unyama uliopitiliza. Huu ni udhalilishaji wa hali ya juu. Hatuwezi kuuvumilia.
Nimeshamuomba Waziri wa Mambo ya Ndani na IGP wachukue hatua stahiki haraka.
Pia nawaomba sana ndugu zangu msiesambaze hizo video. Hiyo ni kuendelea kumdhalilisha huyo dada. Amebakwa na pia wamerekodi hilo tukio! Hii haistahimiliki na haivumiliki. Mwalimu aliwataka wanawake wote na wanaume wapenda haki na maendeleo ya wanawake kukemea kwa nguvu zote unyama huo.

No comments:

Post a Comment