WAKATI
tukiuanza mwaka 2015 ni vema kwa wale tuliyoteuliwa tena kumshukuru mwaenyezi
mungu wa rehema.
Pia
tuwaombee wale waliotangulia mungu akaziweke
roho zao mahali panapostahili kwa vile yeye ndio mwenyekujua udhaifu
wetu.
Nataraji
kuwa mwaka uliopita tulishirikiana vizuri katika kuhabarishana hivyo nivema
mwaka huu wa 2015 ushirikiano ukazidi kupita ule wa awali.
Pamoja
na kuukaribisha mwaka mpya bado watu wenye ulemavu changamoto zao baadhi yake
hazijapatiwa ufumbuzi hivyo ni vema kila mmoja wetu mwaka huu aongeze jitihada
zaidi katika kuwatatulia changamoto hizo.
Niwaombe
watunga sera katika mwaka huu wajaribu kuja na mbinu mpya ambazo zitasaidia
kuwakomboa watu hao kutoka katika unyonge unaokabili.
Licha
ya nasaha hizo leo Safu hii imepata bahati ya kutembelewa na Paulo Ezekiel,
ambaye ni mkazi wa wa Mkoa wa Kilimanjaro.
Kijana
huyu ni mlemavu wa miguu ambao ameupata hivi karibuni baada ya kuugua miguu kwa
kipindi cha zaidi ya mwaka kuanzia
mishoni mwa mwaka 2013.
Kijana
huyo anasema mwanzo wa aliingia Dar es Salaam mwaka 2011, akiwa katika shughuli
zake maeneo ya Kariakoo alianguka ghafla na kupoteza fahamu ndipo alipookotwa
na polisi na kupelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Kwa
kuwa hakuwa na fahamu alipatiwa matibabu ya msaada kutoka hospitali hadi
aliporejewa na fahamu alijikuta miguu yake haina uwezao wa kutembea tena.
mwanzo
ilianza kupata ganzi kwa muda wa miezi mitatu huku akishindwa kutembea matokeo
yakemwaka 2014 akapelekwa Hospitali ya
Taifa Muhimbili ambako alikaa kwa muda wa miezi minne.
Baada
yauchunguzi wa madaktari Ezekiel aligundulika kuwa mishipa ya miguu yake
imepoteza nguvu hali iliyomfanya ashindwe kutembea kama awali.
Kuanzia
hapo akaanza kutembea kwa kutumia magongo huku pia akipewa ushauri wa kufanya
mazoezi.
Kabla
ya kupatwa na ulemavu huo, Ezekiel alikuwa akifanya kazi ya kuongoza wageni
wanaotoka nje ya nchi hapa jijini Dar es Salaam.
Ni
kijana mwenye uwezo wa kuzungumza lugha ya kingereza kwa ufasaha na ndio maana
amekuwa akifanya kazi hiyo kwa mafanikio makubwa.
Hata
hivyo, tangu akumbwe na maradhi hayo hana uwezo tena wa kufanya kazi hali
inayomfanya aishi maisha ya kubahatisha.
Kutokana
na mazingira hayo anahitaji msaada kutoka kwa wasmalia wema na kikubwa
anachohitaji ni msaada wa baiskeli ambayo anaamini kuwa itamsaidia kufanyia
kazi zake na kujipatia kipato.
Ezekiel
ni kijana ambaye anasema hapendi kuomba kwa vile anaona kitendo cha kuomba ni
aibu hivyo akipata baiskeli hiyo atajiepusha na tendo hilo la kuomba.
Pia
kwa dhati anawaomba kwa dhati msaada huo wa baiskeli kwani hawezi kupita
mitaani na kuombaomba hali ya kuwa hana uwezo wa kutembea hivyo nawaomba
wasmalia wema myaokoe maisha yake.
Labda
katika hili ni Vema Watanzania wenye guswa na tatizo la kijana Ezekiel
tujitokeze ili tuweze kumsaidia na amini wapo baadhi ya wadau wenye uwezo basi
ni wakati wao wakujitolea na si kusubiri kutoa misada kwenye maeneo ambayo
wanajua kuwa watapata faida.
Msaada
wa kweli anapewa mtu asiyejiweza hivyo basi kuanzia sasa tujaribu kujenga
utaratibu huo.
No comments:
Post a Comment