KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Monday, 2 March 2015

AZAM FC YATIMUA KOCHA



KOCHA Mkuu wa Klabu ya Azam FC Joseph Omog na Msaidizi wake Ibrahim Shikanda, wametimuliwa rasmi kuinoa timu hiyo kutokana na kushindwa kutimiza matakwa ya mkataba wao.
Akizungumza na Jijini Dar es Salaam leo, Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba alisema, wamefikia hatua hiyo ya kumtimua Omog Raia wa Cameroon na Shikanda Raia wa Kenya kutokana na kukiuka kipengele cha mkataba wao.
Kawemba alikitaja kipengele hicho kuwa ni kushindwa kuipeleka timu hiyo katika hatua ya makundi ya michuano ya Kimataifa ambapo Azam FC ambao ni Mabingwa watetezi waliondolewa na El Merreikh kwa kubugizwa mabao 3-2 baada ya nyumbani kushinda 2-0 huku ugenini wakichapwa bira huruma 3-0.
“Katika makubaliano ya mkataba wetu na kocha huyo na mwenzake kuna kipengere cha kuipeleka timu hatua za mbele zaidi kuanzia makundi lakini cha kushangaza timu haijafanya hivyo, basi tumeamua kuachana nao Omog na Shikanda,”alisema na kuongeza kuwa timu hiyo itaendelea kunolewa na kocha msaidizi George Nsimbe mpaka kumalizika kwa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Hata hivyo habari za ndani ambazo Blog ilizipata jana kutoka ndani ya klabu hiyo aliyekuwa Kocha Mkuu wa Simba Patric Liewig anatajwa kurith mikoba ya Mcameroon huyo ambaye alichukua kijiti cha Stewart Hall.

No comments:

Post a Comment