KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday, 10 April 2015

JAJI RAMADHAN: HAKUNA HAKI YA MTU KUKATAA KUTII SHRIA

RAIS  wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Haki za watu Mhe Agustino Stephen Ramadhan amesema kuwa hakuna haki ya mtu kukataa kutii Sheria na kuwataka wananchi  kujiepusha na vitendo vya  kujichukulia sheria mikononi mwao .
 
Amesema kuwa katika nchi yenye misingi ya Utawala Bora jamii inapaswa kuiachia mahakama kutoa tamko juu ya mambo ambayo  yanakinzana na jamii kwa lengo la kuhakikisha kwamba jamii inapata haki kwa mujibu wa sheria .
 
Akizungumza kwenye  mahafali ya tatu ya wasaidizi wa sheria wa majimbo  Zanzibar yaliyofanyika kwenye ukumbi wa ZSSF nje kidogo ya Mji wa Chake Chake , amesema kuwa mahakama ndio chombo ambacho kinatafsiri  sheria na kutoa haki .
 
Rais huyo ambaye pia Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu Tanzania ametumia fursa hiyo kuwataka wasaidizi wa Sheria kuwahudumia wananchi wanyonge kuweza kupata haki zao na kujiepusha kutumia elimu waliyoipata kwa maslahi yao binafsi .
 
“Hakuna uhuru wa mtu kukataa kutii sheria , hivyo jamii mnakiwa kutojichukulia sheria mikononi mwao bali waiache mahakama kutoa tamko juu ya masuala yanayoikinza jamii kwa lengo la kulinda amani ” alisisitiza .
 
Aidha amepongeza juhudi zinazochcukuliwa na kituo cha sheria  Zanzibar kwani kimeweza kuleta mawimbi ya matumaini kwa jamii na kubomoa ukuta wa maovu , wanyinge pamoja na maonevu wanayofanyiwa wananchi hasa maskini.
 
Amefahamisha kwamba katika misingi ya demokrasia na utawala sheria uhuru wa maoni ya wananchi unazingatiwa na kuongeza kwamba taasisi binafsi zinaweza kuchangia kuongezeka  kwa uhuru wa wananchi .
 
“Kituo cha huduma za sheria Zanzibar imekuwa ni moja ya taasisi ambazo zinachangia kukua kwa uhuru wa maoni wa  wananchi hasa katika nchi zinazofuata utawala wa Sheria ” aliongeza Jaji Agustino Ramadhan .
 
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini wa kituo cha huduma za sheria Zanzibar Pr Chris Maina Pita amesema kuwa kituo hicho kimekuwa mstari wa mbele kuwaelimisha wananchi elimu ya Sheria ili waweze kuisaidia jamii yao inayowazunguka .
 
Amesema kuwa kituo hicho kimeanda motisha kwa wasaidizi wa sheria wanaofanya vizuri katika masomo yao na ambao wanataka kujiendeleza zaidi kusoma Elimu wa Sheria kwamba kinadhamini gharama za masomo wa wanafunzi hao katika chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali .
 
“Kituo kimeandaa mfuko kwa ajili ya wanasaidizi wa Sheria ambao wanataka kujiendeleza zaidi kielimu katika vyuo vikuu , chuo kinagharamia gharama za masomo kwa wanafunzi hao , na tayari wafadhili wameanza kuingi a fedha katika mfuko huo ” alifahamisha .
 
Mapema Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Harusi Miraji Mpatani amesema kuwa tayari kituo hicho kimetoa wasaidizi wa Sheria 197 huku wengine 82 wakiwa wanaendelea na masomo yao .
 
Mpatani ameeleza kuwa kituo kinaridhiwa na utendaji wa kazi wa wasaidizi hao wa Sheria wa Majimbo Zanzibar kwani wameweza kusaidia wananchi kupata haki .

No comments:

Post a Comment