KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday, 3 April 2015

WANDISHI WAPATA MAFUNZO YA UFUGAJI WA KUU

Msimamizi wa Mradi wa Mkulima Mbunifu Nchini, Ayubu Nnko
  NA MWANDISHI WETU

WAANDISHI wa vyombo mbalimbali vya habari nchini wamepatiwa mafunzo ya jinsi ya kuandika habari za kilimo cha ufugaji wa kuku ambao utampatia maarifa msomaji anayetahitaji kufuga kuku kwa mara ya kwanza.

Mafunzo hayo ya siku mbili yalitolewa na Mradi wa Mkulima Mbunifu, ambao unasimamiwa na Biovision Africa Trust, yalifanyika mkoani Arusha mwanzoni mwa wiki hii.

Mradi wa Mkulima Mbunifu ni mradi wa mawasiliano, ambao kwa namna moja au nyingine unaeneza na kutoa elimu ya kilimo endelevu kwa wakulima nchini na nchi za jirani.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo juzi, Msimamizi wa mradi huo nchini, Ayub Nnko, alisema anaamini mafunzo hayo yatawasaidia waandishi hao, kuandika habari za ufugaji kwa usahihi bila ya kuacha maswali kwa wadau wa kilimo.

Alisema waliamua kutoa mafunzo hayo baada ya kubaini upungufu wa uandikwaji wa habari za kilimo cha ufugaji kama vile wa kuku, ambapo kila wakulima walipozisoma walibaki na maswali.

“Sasa ninaamini baada ya mafunzo haya  utakuwa mwanzo mzuri kwa nyie washiriki kwenda kuandika na kuwafikishia taarifa sahihi ambazo zitawasaidia wakulima na wafugaji na kuifanya shughuli hiyo kuwa rahisi kwao,” alisema Nnko.

Nnko aliwasihi  wananchi kuacha kukidharau kilimo, kwani maisha ya kila mwanadamu hayawezi kuendelea bila kuhusisha kilimo ambacho kimekusanya mambo mbalimbali ikiwemo ufugaji.

Watoa mada katika mafunzo hayo walikuwa ni John Cheburet na Caroline Nyakundi kutoka Kenya, ambao walisema mradi huo ambao unafadhiliwa na Biovior Fundation for Ecological, Switzerland, unaendeshwa kwa ushirikiano wa nchi hizo mbili. 

Mradi huo nchini Kenya umeanzishwa mwaka 2010 kisha mwaka 2011ukaingia Tanzania.

No comments:

Post a Comment