WIZARA ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na ‘World Lung Foundation(WLF)’, zimezindua kampeni ya uzazi wa mpango mkoani Kigoma.
Kampeni hiyo inakuja baada ya mkoa huo kuonekana bado uko
nyuma kielimu kuhusu mpango huo ukilinganisha na mikoa mingine.
Mganga Mkuu wa Mkoa waKigomba Dk. Leonard Subi, ambaye
alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, alisema mpango huo umeanza jana na
kwamba utakamilika Agosti mwaka huu huku akibainisha kuwa umekuja wakati
muafaka.
Alisema kampeni hiyo ya uzazi wa mpango itasidia kuokoa
maisha ya akina mama kutokana na matatizo ya kiafya, kuzaa watoto walemavu na
vifo ambavyo vinaweza kuchangiwa na kupasuka kwa kizazi kwa sababu ya kuzaa
watoto bila ya utaratibu.
Dk. Subi, alisema kufanikiwa kwa mpango huo kutasaidia
familia nyingi kuwa na afya bora ambayo itawasaidia katika shughuli za
kujizalishia kipato.
“Ukosefu wa mpango wa uzazi, ikiwemo kuacha nafasi kati ya
mimba moja na nyingine inachangia kuongeza vifo vya akina mama na watoto
wachanga nchini,”alisema Dk. Subi.
Alisema kiwango cha uzazi Kanda ya Magharibi ikiwemo Kigoma
ni watoto saba ikilinganishwa na wastani wa watoto watano kwa Tanzania na
wastani wa watoto 2.5 duniani.
Naye Mkurugenzi waTaifa wa WLF, Dk. Nguke Mwakatundu,
alisema kampeni hiyo inajulikana kwa jina la Thamini Uhai, iliyoanza mwaka 2014
ilitilia mkazo muhimu wa kujifungua katika kituo cha afya.
Alisema data iliyotolewa hivi karibuni na Shirika la Afya
Duniani (WHO), inakadiria kuwa ingawa mwaka 2010 idadi ya vifo vya akina mama
nchini ilikuwa asilimia 3 ya vifo vyote vya uzazi duniani.
No comments:
Post a Comment