![]() |
| Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Maramba |
MSEMAJI wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Adrian Serine amesma Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Felchesmi Mramba, hajahudhuria wa wala kuandaa mkutano wowote wakisiasa.
Severine, alisema hivyo
wakati alipokuwa akikanusha taarifa zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii juzi
kwamba Mkurugenzi huyo, alikuwa miongoni mwa wajumbe 17 wanaodaiwa kuandaa moja
wapo ya mikutano ya kisiasa katika
hoteli ya Kibo Palace jijini Arusha.
Akizungumza jijini Dar es
Salaam jana, msemaji huyo, alisema ingawa taarifa hiyo haikufafanua jina la mkurugenzi
mtendaji huyo wa Tanesco, kwa kutoweka wazi, zinaamanisha ni Mramba hivyo
shirika linawataka wananchi kuzipuuza kwani sio sahihi na zinalenga kumharibia
mkurugenzi huyo.
“Katika taarifa hii haijulikani
kama mkurugenzi mtendaji ni nani
anayetajwa kwani kiongozi mkuu wa tanesco hajatanjwa jina basi taarifa hizi
zinamaanisha mkurugenzi mtendaji ambaye ni basi si sahihi,”alisema Severine.
Alisema, hivyo kwa vile Mei 29 mwaka huu, inayotajwa
katika taarifa hiyo Mkurugenzi Mtendaji alikuwa na mkutano wa wafanyakazi wote wa makao makuu ya shirika hilo na wa
mikoa ya Dar es Salaam na Pwani kuanzia saa 7:00 mchana hadi saa 12:00 jioni , uliofanyika
Ubungo na kwamba Mkurugenzi huyo asingeweza wakati huo huo kuwapo mjini Arusha.
Severine alisema kuwa
Mkurugenzi huyo Mei 30 alisafiri kikazi nje ya nchi ambako hadi sasa hajarejea
nchini.
Aidha, mkurugenzi wa tanesco ni mtumishi wa umma anaongozwa na
kanuni za utumishi wa umma zinazomtaka kutojihusisha kwa namna
yoyote na masuala ya kisiasa, kanuni
ambazo mkurugenzihuyo anazifahamu vizuri.
Severine alisema kutokana
na kanuni hizo, anaamini kuwa mkurugenzi huyo asingeweza kufanya hivyo, kwani kufanya
hivyo ni sawa na kwenda kinyume na maadili ya utumishi wa umma.
“Ikumbukwe kuwa Tanesco ni
shirika la kiufundi na lipo kwa manufaa ya Watanzania wote,’alisema Severine.
Aliongeza kwa kusema kuwa
mkakati wa shirika kwa sasa ni
kushughulikia changamoto za umeme nchini na kuhakikisha nchi ina umeme wa
uhakika, mkakati ambao ambao mkurugenzi mtendaji ndiye msimamizi wake.

No comments:
Post a Comment