![]() |
| Baadhi ya Wanalyalamo wakijumuika na watoto wa Kituo cha Yatima Group Trust Fund. |
WITO umetolewa kwa Watanzania
kujitolea kwa hali na mali kusaidia watu wenye uhitaji maalumu ikiwemo watoto
yatima wanaolelewa katika vituo vituo malimbali.
Wito huo umetolewa jijini juzi,
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Yatima GroupTrust Fund kilichoko Chanika, Dar
es Salaam, Winfrida Lubanza, wakati alipozungumza na wanafamilia wa Lyalamo.
Alisema jamii inapaswa
kuwakumbuka watoto walioko katika vituo hivyo kwa vile wanastahili kupata
mahitaji ya kibinadamu kama ilivyo kwa watoto walioko majumbani.
“Watoto yatima ni watoto kama
wengine nao wana uhitaji sawa hivyo jamii isiwasahau na kwani nao wanapata faraja
na kupata matumaini zaidi wanapokumbukwa,”alisema.
Aliongeza kwa kusema kuwa kituo
chake kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo chakula, dawa, sabuni na
ada kwa wanafunzi sambamba na mtaji wa kuwezesha kuanzisha biashara ambayo
itaweza kuwapatia fedha za kujikimu.
“Tuna changamoto nyingi mfano kuna
mwanafunzi ambaye yuko kidato cha nne amerudishwa kituoni kwa sababu hatujakamilisha
ada,”alisema.
Naye kiongozi wa Lyalamo Family,
Aziza Kibwana, alisema wamefarijika kufika kituoni hapo na kujionea changamoto
hizo, watajitahidi kuchangia walichojaliwa.
Pia alisisitiza wadau wengine
kujitokeza katika kusaidia vituo vinavyolea watoto hao, baadhi yao watakuwa
wataalamu wa kesho katika taifa hili.
“Sisis tumesoma shule ya msingi
boarding tukiwa wadogo na tulikuwa na watoto kutoka katika vituo kama hivi
hivyo tunaguswa sana na hali zao ndio maana tuko hapa.
Humu kuna marais, kuna wabunge,
wanasoka, wasanii, wafanyabiashara, madaktari, wahasibu nakadharika sasa ni
muhimu kuwakumbuka na watoto walioko huku ili kuwajengea misingi mizuri yay a
kutimiza ndoto zao,”alisema.
Katika ziara yao hiyo walikabidhi
kituo hicho vyakula, mafuta, dawa, madatari, sabuni na vitu vingine ambapo
watoto walioko kituoni hapo walifurahi na kushukuru.
Kituo hicho kilianzishwa mwaka
2001, hadi sasa kinalea watoto kati ya150 hadi 300 wenye umri wa kuanzia mwaka
0 hadi miaka 18.

No comments:
Post a Comment