| Katibu Mkuu wa Chama cha Kijamii (CCK), Renatus Muabhi (katikati). |
MKUTANO
wa kusaini maadili ya uchaguzi kati ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Vyama
vya Siasa, kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Otoba 25 mwaka huu umevunjika baada ya
vyama kupinga kusaini kutokana na kunyofolewa baadhi ya kurasa katika kitabu
cha maadili hayo.
Kwa
mujibu wa maadili hayo, kila Chama Cha Siasa na kila mgombea atawajibika
kusaini maadili hayo, chama ambacho hakitasaini kitazuiliwa kushiriki katika
kampeni za uchaguzi.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Katibu Mkuu wa Chama Cha Kijamii
(CCK), Renatus Muhabhi, alisema vyama hivyo vimeitaka NEC kuacha mzaha na suala
la uchaguzi.
Muhabhi,
alisema baada ya hoja hiyo wajumbe wote wakaunga mkono hoja hiyo, ikabidi
Mkurugenzi wa NEC, agize yakaletwe lakini cha kushangaza yalipoletwa ikabainika
kulikuwa na upungufu wa kurasa 10 katika ya 24.
Muhabhi,
alisema pamoja na sintofahmu hiyo, Mkurugenzi wa NEC, alishindwa kuwaeleza
wajumbe sababu haswa zilizofanya kuosekana kwa kurasa hizo na ilikuwa ni kwa
maslahi ya nani.
Alisema,
baada ya mvutano huo wajumbe wote kwa pamoja waliungana na kuamua kuvunja kikao
hicho huku wakiitaka Tume kuwa inahakikisha kuwa inayafikisha makubaliano ya
awali kabla ya kutiwa saini Jumatatu ijayo.
Katibu
Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Philp Mangula, alifoka na kusema kwamba
serikali imekuwa ikilaumiwa kutokana na uzembe wa mtu mmoja.
Mangula, alisema inaonekana Mkurugenzi alikuwa
haijajipanga kwa hiyo amekurupuka hivyo basi
wajumbe wanapaswa waeleze kilichotokea sababu iliyosababisha hali hiyo.
Mkurugenzi
wa Idara ya Kampeni na Uchaguzi wa NCCR-Mageuzi, Faustine Sungura, alisema
ilibidi wavunje mkutano huo baada ya Katibu Mkuu wa CCK, Muhabhi kuibua hoja ya
kutaka waletewe fomu za vikao viwili vilivyopita.
“Kwa
kweli kitendo hicho kilimsikitisha Katibu Mkuu wa CCM, ambaye aliwalaumu kwa
kuwaambia ndio Tume kwamba wanasababisha serikali ilaumiwe kama, walikuwa
hawajajiaandaa ilikuwaje watuite,”alisema Sungura.
Sungura,
alisema baada ya Mkurugenzi hatua hiyo imemkasirisha Mangula, alionekana kuwa
karibu na katibu mkuu huyo, mithiri ya mtu aliyekuwa akitaka kuomuomba radhi.
“Tulika
kama dakika 25 muda wa kuwasubiri kwa ujumla mazungumzo yote yamechukua muda
huo, inasikitisha kwani kulikuwa kumekosekana karatasi kama 13,”alisema
Sungura.
Mkurugenzi
wa NEC, Julius Malaba, alipotakiwa kuzungumzia kadhia hiyo alijibu kwa sauti ya
upole na kwa kifupi kwamba mkutano huo haukuvunjika bali ulikuwa umeahirishwa
na kitaendelea Jumatatu ijayo.
Hata
alipotakiwa kutoa sababu za kuahirishwa mkutano huo ndani ya dakika 25 tangu
kuanza: Haujavunjika ni nani aliyekwambia kama ni sababu waulizeni hao
waliowaeleza, lakini kikao tumekiahirisha.
Kwa
upande wake Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mstaafu Hamid
Mahmoud Hamid, aliwaomba radhi wajumbe baada ya kuambiwa na Mangula kwamba
walikuwa hawajajipanga na ndio maana mkurugenzi anafanya kazi za hovyo hovyo.
Katika
Mkutano huo Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damiani Lubuva hakuwepo katika mkutano huo
ikidaiwa kuwa yuko nje ya nchi.
No comments:
Post a Comment