KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Thursday, 4 February 2016

WAKILI WA AMIR WA UAMSHO SHEUKH FARI HAD ASEMA MTEJA WAKE HAUNGI MKONO KURUDIWA UCHAGUZI ZANZIBAR



SHEIKH Mkuu wa Baraza Kuu la Waisilam (Bakwata), mkoani Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum huenda akaingia matatani kutokana na kauli yake kuwa kiongozi wa Uamsho, Amir Farid Had Ahmad, ameunga mkono kurudiwa kwa uchaguzi Zanzibar.
Juzi wakati akizumgumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam juu ya mkwamo wa kisiasa unaondelea Zanzibar, Alhad Salum, alisema kwa sasa njia pekee ya kumaliza mgogoro huo ni kurudiwa uchaguzi, kwani hata Amir wa Uamsho Sheikh Farid Hadi Ahmed pia anaunga mkono.
 Akizungumza jijini leo, Wakili, Juma Nassor,  alisema hayo wakati alipokuwa akitoa ufafanuzi kuhusu ukweli wa mteja wake, Sheikh Farid kama kweli ameandika barua hiyo ya kuunga mkono, iliyooneshwa mbele ya wandishi wa habari kama na Sheikh Alhad Salum.
Nassor, alisema Sheikh Alhad Salum, anaweza kuingia matatani endapo kama Sheikh Farid, atalalamika na kulifikisha  kwenye vyombo vya sheria madai hayo kutokana na taarifa hizo kutangaziwa Umma kwamba aliandika barua iliyokuwa na mambo matatu moja likiwa hilo la kuunga mkono kurudiwa uchaguzi.
“Kuhusu nini kifanyike kutokana na kitendo cha Alhad Salum, hiyo itategemena na Sheikh Farid mwenyewe kama atamua kufikisha malalamiko kwenye vyombo vya sheria lakini pia anaweza kuamua kusamehe, uamuzi ni wake,”alisema Nassoro
 Hata hivyo, wakili huyo, alisema kuwa viongozi wa  Chama Cha Mapinduzi (CCM), tayari wamekwishasema kupitia majukwaa ya siasa kwamba Zanzibar ni nchi iliyotawaliwa baada ya kufanyika mapinduzi hivyo haiwezi kutolewa kwa njia ya makaratasi yaani uchaguzi.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini juzi Siku ya Jumanne, , Alhad Salum, alisema kusudi kubwa la kukutana nao ilikuwa ni kutoa salam za pongezi kwa serikali ya awamu ya tano kutokana na kitendo chake kuimarisha nidhamu kwa watumishi wa Umma na wale wa serikali.
Alisema, Bakwata, imefikia hatua hiyo baada ya kubaini kuwa hakuna njia mbadala ya kumaliza gogoro huo, zaidi ya kurudiwa uchaguzi.
“Kwa sasa  hiyo ndiyo njia pekee ya kumaliza mgogoro huo, kwani hakuna njia mbadala hata Amir wa Uamsho Sheikh Farid Hadi Ahmed pia anaunga mkono suala la hilo la kufanya uchaguzi wa marudio kwa mujibu wa barua yake aliyonitumia mimi toka Gerezani. 
Hivyo basi naomba kuchukua fulsa hii kukiomba Chama cha Wananchi (CUF),  amabacho tayari kimekwishatangaza kususia uchaguzi huo wa marudio na Vyama vingine vyote vya siasa vilivyoko Zanzibar viache kususia uchaguzi huo,”alisema Alhad.
Alisema baadala ya kususia uchaguzi huo ni vema vikajipanga kwa ajili ya kushiriki na huku akiomba ZEC kuhakikisha kuwa inasimamia uchaguzi huo kwa kuzingatia haki, uadilifu na umakini mkubwa kwa masilahi ya Taifa.
 “Tunawaomba Wazanzibar wadumishe amani na utulivu walionao na kulinda umoja na mshikamano wao kwa kuwa wao ni ndugu,”alisema Alhad.
Kazungumzia mafanikio ya serikali ya awamu ya tano, Alhad alisema anaipongeza kutokana na dhamira yake ya kubana na kupunguza matumizi ya serikali yasiyokuwa ya lazima na baadala yake kuelekeza fedha kwenye huduma za kijamii.
 Alisema kutokana utaratibu huo, tayari Watanzania wameanza kunufaika na huduma kama vile suala la elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne huku akibainisha kuwa ni jambo jema linalopaswa kupongezwa.
“Kwa kuwa ada za shule na gharama za kuandikisha watoto wanaoanza darasa la kwanza ulikuwa mzigo mkubwa kwa wananchi walio wemgi, pamoja na kuboresha huduma za Afya kwenye Hospitali za serikali,”alisema Alhad.
 Alisema pamoja na pongezi hizo lakini pia Bakwata inaiomba serikali izidi kupambana na changamoto mbalimbali hasa zote zilizoko ndani ya jiji hilo hususan suala zima la foleni ambalo linachangia kuzorotesha uchumi wa Taifa.
 Alhad, alisema pia kuna haja kwa serikali kumaliza mvutano uliyojitokeza kati ya wadau wa usafirishaji na Sumatra juu ya kiwango cha nauli za Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (DARTS).
 Alhad, alisema anaamini kuanza kwa mradi huo kuna weza kuwa mkombozi katika kupunguza changamoto hiyo ya foleni katika jiji hilo.  

No comments:

Post a Comment