KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday, 22 April 2016

MUBUMDA, KAGERA WALILIA MAJI YA BOMBA


WAKAZI wa Kijiji cha Mubunda wilayani Muleba mkoani  Kagera wameilalamikia serikali kutokana na kushindwa kukamilisha kwa wakati mradi wa maji ili waweze  kuondokana na adha wanayoipata ya kufuata huduma hiyo mbali.
Wakazi hao waliyasema hayo baada kuona mradi huo wa maji uliyoanzishwa Januari mwaka 2014, ulitakiwa kukamilika Januari mwaka jana kushindwa kukamilika kwa wakati kama ilivyokusudiwa.
Ujenzi wa mradi huo ambao ulitarajiwa kumaliza kero ya wananchi kuhangaikia huduma hiyo huku wakitumia maji ambayo ni hatari kwa afaya zao, umeigharimu serikali sh.Milioni 900.
Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi, kwa niaba ya wakazi wenzake aliyongozana nao, James Muga alisema pamoja kudaiwa kuwa mradi huo umekamilika kwa asilimia 99, hata hivyo, wakazi hao hawaamini kama ujenzi huo unalingana na thamani ya fedha iliyotumika katika ujenzi wake.
Alisema, hatua ya kuuzungumzia mradi huo kupitia vyombo vya habari kumesababishwa na wasimamizi wa utekelezaji wa mradi huo kushindwa kutoa sababu halisi zinazo kwamisha kukamilika mradi huo ambao ujenzi wake ulipangwa kuwa wa mwaka mmoja na ambao umeishapita tangu januari mwaka jana.
“Hatuelewi sababu inayokwamisha mradi huu, wanatuambia mradi umekamilika kwa asilimia 99 lakini tangu tulipoambiwa mwaka jana hadi sasa mwaka mmoja umepita tunashangaa haujaanza kutoa huduma iliyokusudiwa.
“Wakati wakiendelea kutoa sababu zinazojichanganya kwamba mara mradi umekamilika asilimia 99 kilichobaki ni kuzinduliwa lakini pia utasikia hivi sasa wanasubiri hela za kununulia mashinde za kusukuma maji sasa hatuelewi tushike lipi lakini yoye kwa yote wananchi ndiyo tunaoathirika kwa kukosa huduma hiyo muhimu,”alisema Muga.
Akitolea ufafanuzi malalamiko hayo Diwani wa Kata Mubunda, Kalinjuma Kamili, alisema mradi huo hadi sasa umefikia asilimia 85 na wala siyo 99, kilichojitokeza ilikuwa ni kukosekana kwa mashine ya kusuma maji.
“Unajua awali mradi huo ulipangwa itumike mashine ya kusukuma maji lakini baadaye ulipokuja umeme wa REA ndiyo wakaona siyo vizuri kutumia mashine kwa sababu umeme ni bora zaidi,”alisema Kalinjuma Kamili
Kalinjuma Kamili alisema baada ya makubaliano kati ya Mkurugenzi na Mkandarasi ya kubadili mfumo wa awali tayari kwa siku ya jana mkandarasi imekwishaanza kufunga vifaa hivyo vinavyotumia umeme kwa hiyo wakikamilisha huduma hiyo itaanza kupatikana kuanzia leo.
“Kweli kulikuwa na changamoto iliyosababisha kuchelewa mradi huo ili kuwa ni kukosekana kwa fedha na siyo mradi huu pekee bali ilikuwa yote iliyokuwa ikifadhiliwa na Benki ya Dunia ilisimama,”alisema.
Kuhusu, kujengwa chini ya kiwango, Kalinjuma Kamili, alisema hawezi kukbaliana na kauli ya wakazi hao, kwa sababu hatua zote za ujenzi zilizokuwa zikifanyika alizishuhudia lakini pia Mkurugenzi alikuwa anapitia kila hatu wakati ujenzi wa mradi huo ilipokuwa ukiendelea.
Alisema, anaweza kukubali hilo baada ya kufungwa mashine hizo, nakushindwa kutoa maji hapo ndiyo anaweza kukubali lakini kwa sasa hakubalini na hilo kwa vile tangu hatua za ujenzi wa matenki na kulazwa kwa mabomba alishuhudia kwa kuwa bega kwa bega na makandarasi.
WISHO    


No comments:

Post a Comment