KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday, 27 February 2015

POLISI WALAUMIWA DAR

WAKAZI wa jiji la Dar es Salaam wameshangazwa na ukimya wa uongozi wa Mkoa huo, wa kuvifumbia macho vitendo vya kinyama vinavyofanywa na polisi wakati wa wanapofanyakazi ya kukamata pikipiki (Bodaboda), wafanyabiashara ndogondogo (Wamachinga) na Mamalishe.
Hatua ya kukamata bodaboda inatokana na agizo la mkuu wa mkoa huo ambalo linawataka madereva wa bodaboda kutoingia akatikati ya jiji ambalo amelitoa zidi ya miezi mitano iliyopita.
Wakizungumza na BLOGG hii jijini leo, walisema vitendo wanavyofanyiwa madereva wa bodaboda, inasikitisha kwani vinakiuka haki za binadamu.
Kwa niaba ya wenzake, Jafari Yahya, alisema kutokana ukimya huo, wakazi haowanamuomba waziri mkuu mizengo pinda kuchukua hataua za haraka ili kukomesha vitendo hivyo ambavyo vimekithili.
Alivitaja vitendo hivyo kuwa ni kuporwa mali za wafanyabiashara hao pia kuumizwa madereva wa bodaboda pamoja na abiria wanaopakia kutokana na kukimbizwa hovyo bila kujali sheria za usalama barabarani wakati polisi wanapotaka kuwakamata.
“Ukiangalia askari hawa, moja kwamoja utaona wanalitumia agizo la mkuu wa mkoa kama kigezo cha kujihalalishia kufanya unyang’anyi wa mali za walala hoi hawa ambao wamepigika kimaisha,”alisema Yahya.
Yahya, alisema mamalishe, bodaboda na wamachinga wamekuwa hawana raha kutikana na kuporwa mali zao mchana kweupe kigezo ikiwa ni agizo la mkuu wa mkoa, hali ambayo inawafanya wananchi wanaoshuhudia matukio hayao kuungana na wafanyabiashara hao kuichukia serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Aidha, alidai kuwa polisi hao wamekuwa wakifanya kazi hiyo bila ya kuwa na muda maalum mfano utawaona majira ya saa 12:00 jioni wakikamata mali za watu kama vile nguo, mabegi na simu na kichoshangaza wanaondoka nazo mbio katika gari bila ya mwenye mali.
Alisema, akama serikali haitakuwa makini na chuki na hasira zinazozidi kuongezeka dhidi ya vitendo wanavyofanyiwa huku serikali ikiwa kimya kuna hatari uvumilivu wa wananchi siku moaja ukaja kutoweka na kitakachotokea wakati huo hakitajulikana.
“Kinachofanywa na polisi ni wizi, unyang’anyi ambao uko sawa na ule wakutumia nguvu kwani wanakuja na silaha na gari wanachukuwa mali zaraia ambao hawana silaha na kutokomea nazo kusikojulikana.
“Wafanyabiashara hawa hawajamdhulu mtu mwingine, ni ajabu kama mtu anajitafutia kipato kwa uhalali halafu vyombo vya doala vinawapinga kwa kweli sheria hiyo tunaishangaa sana,”alisema Yahya.


No comments:

Post a Comment