KIGOGO mmoja wa Wakala
wa Majengo Tanzania (TBA), inadaiwa kuwa amengia kwenye kashfa ya kutumia njia
za udanganyifu katika kujipatia wadhifa alionao sasa.
Chanzo cha kuaminika
kutoka ndani ya ofisi hiyo, kililiambia BLOG hii, kuwa udanganyifu huo
umetokana na mchakato mzima uliyomfanya kigogo huyo apate cheti baada ya
mtihani uliyofanyika mwaka 2012 unatia shaka.
Kilisema kuwa kigogo
huyo, alijipatia cheo hicho bila ya kufuata utaratibu unaotakiwa ikiwa ni
pamoja na kuwasilisha cheti toka Bodi ya Usajili wa Wasanifu na Wakadiriaji wa
Majengo katika tume ya ajira, wakati vyeti vya watahiniwa waliofaulu
vikiwahavijatoka.
“Mitihani ilifanyika
Juni 2012 na matokeo yametangazwa Julai 31, 2012 na vyeti vikiwa havijaandaliwa
lakini yeye aliwakilisha cheti Juni kabla
ya vyeti kutolewa kitendo kilichomfanya ajipatie cheo kwa udanganyifu.
“Pia kutokana na
elimu yake hakuruhusiwa kufanya mtihani wa mwisho kabla ya ‘Intermediate’ lakini kwa mshangaao Bodi ikamruhusu hivyo
kukiuka sheria na taratibu za usajili.
Chanzo hicho
kilisema Msajili wa zamani wa Bodi Architect, Meresi alimzuia asifanye mtihani
wa ‘Final’ bali alitakiwa aanzie na ‘Intermediate’ lakini alifanya mtihani huo
katika mazingira yenye utatanishi, ili tu apandishwe cheo isivyo halali.
Uwamuzi wa
Architect, Meresi kuzuia kigogo huyo kulijenga chuki kati yake na Waziri wa
Ujenzi kwa vile waziri huyo anadaiwa kuwa alikuwa karibu na kigogo huyo.
“Chuki hii
ililimfanya waziri huyo wa ujenzi kumtukana Architect, Meresi alipokwenda
kwenye semina ya Bodi Morogoro,”Kilisema chanzo hicho.
Aidha kigogo huyo
aliamua kununua samani zenye thamani ya sh milioni 40, ambazo alidai kuwa
zilikuwa za Rest-House ya Ujenzi Dodoma wakati haikuwa kweli.
Chanzo hicho
kilisema, kumbe samani hizo ili kuwa ni kwa ajili ya kulipa fadhala kwa waziri wa
ujenzi ambaye ametumia madaraka yake vibaya ya kumpatia kigogo huyo cheo hicho
bila ya kufuata taratibu.
“Samani hizo pamoja
na jakuzi lenye Luninga, kwa kujua kitendo hicho siyo halali samani hizo
zilisafiriswa usiku na gari T 246 ANU mali ya Wakala Mkoa wa Dar es Salaam
likiendeshwa na dereva (Jina tunalo na namba yake ya Simu).
“Samani hizo
zilipokewa na mmoja wa vigogo wa TBA Dodoma (jina na namba yake yasimu tunavyo),
ambaye baadaye alizipeleka numbani kwa Wzairi,”kilisema Chanzo hicho.
Aidha, juhudi za
kumpata kigogo huyo zinaendelea ili aweze kutoa ufafanuzi kuhusu madai hayo na
mengine ambayo yanahusiana na utoaji wa nyumba kwa kutumia kigezo cha ukabila.
No comments:
Post a Comment