KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday, 15 March 2015

DAWASCO YAANDAA DAWATI MAALUMU KUSIKILIZA WATEJA WAKE

NA MWANDISHI WETU
SHIRIKA la Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (Dawasco), limeandaa madawati ambayo yatatumika kupokea malalamiko na kutoa elimu katika maadhimisho ya Wiki ya Maji inayoanza leo hadi Machi 22 Mwaka.

Taarifa iliyosambazwa kwa vyombo vya habari ikisainiwa na Ofisa Uhusiano wa Dawasco, Everlasting Lyaro, alisema  madawati hayo yakuwepo katika Ofisi zake za Makao Makuu zilizoko barabara ya Sokoine Drive, Kinondoni na Boko.

 Kaulimbiu ya wiki ya maji ya mwaka huu inasema ‘Maji kwa Maendeleo Endelevu’

Lyaro, alisema licha ya kutoa elimu pia itapokea maoni ya wateja lengo likiwa kuwaelimisha wananchi wa mkoa huo kuhusu sera ya maji.
“Kuna program zinazoenelea za ujenzi wa miradi ya maji, mipango ya baadaye na umuhimu wa ulinzi wa miundombinu ya maji na matumizi sahihi ya dira za maji,”alisema Lyaro.

Alisema madwati hayo yakuwa wazi katika pindi hicho cha wiki nzima kuanzia Machi 16 hadi Machi 22 mwaka huu, kuanzia saa 2 Asubuhi hadi saa 12 jioni kila siku.

 ”Tunawakaribisha wananchi kutembelea ofisi zetu na kuelewa mikakati ya kuboresha huduma za maji iliyopo pia kutoa malalamiko na maoni yao yatakayotuwezesha kujipanga na kuwapatia huduma bora zaidi.

 “Madawati haya yanahudumiwa na wafanyakazi wetu kutoka vitengo mbalimbali  tuna imani wateja wetu na wananchi kwa ujumla watakaotembelea ofisi zetu katika wiki hii ya maadhimisho ya maji watapata elimu kutosha kuhusiana na huduma zetu na taarifa zinazohusiana na sekta ya maji kwa ujumla,”alisema Lyaro.

No comments:

Post a Comment