NA MWANDISHI
WETU
KAMPUNI ya
Bharti Airtel imemteua Balozi Juma Mwapachu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi ya Airtel Tanzania.
Balozi Mwapachu
ni Katibu Mkuu aliyepita wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, nafasi aliyoishika
kati ya Aprili 2006 na Aprili 2011.
Kabla ya uteuzi huu, Mwapachu alikuwa Balozi Mwakilishi Ufaransa na
UNESCO.
Akizungumzia
uteuzi huo mjini Nairobi, Kenya juzi, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Airtel Afrika,
Christian de Faria, alisema ni faraja kwao Balozi Mwapachu kuiongoza Bodi yao
ya Wakurugenzi
Tanzania, kwani ana uzoefu mkubwa utakaoongeza thamani kubwa kwa
bodi yao.
Kwa upande
wake, Balozi Mwapachu alisema mepokea kwa heshima kubwa fursa hiyo na
atashirikiana na wajumbe wenzake wa bodi hiyo kujenga kampuni thabiti yenye
misingi imara, ili kuendelea kutoa
huduma bora ya mawasiliano nchini Tanzania.
“Ukuaji wa teknolojia ya hali ya juu na
ubunifu katika masoko ikisaidiwa na mfumo mzuri wa usimamizi wa sekta hii ni
dhahiri kutakuwa na uwezekano kwa sekta hii kuendelea kutoa mchango mkubwa kwa taifa,” alisema.

No comments:
Post a Comment