Kikwete,
alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Studio
ya kampuni ya Azam Media Group Limited, ambayo ni ya kisasa katika ukanda huu
wa Afrika Mashariki.
Hadi
kukamilika kwa ujenzi wa studio hiyo umegahrimu sh bilioni 53.
Alisema
hivyo kwa vile televisheni hiyo hivi sasa itaonekana kimataifa, hivyo isije
ikawafanya wakashawishika kuwasahau Watanzania na kuanza kurusha vipindi ambavyo
vitakwenda kinyume na sheria za nchi.
Aidh,
alisema serikali haitaona haya, lazima itasema pindi itakapoona baadhi ya
vyombo hivyo habari vinatoa bari za hovyo, ambazo msingiwake ni kuipotosha
jamii na atakayekwenda kinyume lazima atabawa na sheria.
Kikwete, alisema bado serikali inatambua
mchango mkubwa wa vyombo vya habari katika jamii, akiahidi kuwa itaendelea
kuweka mzingira mazuri ya uwekezaji katika sekta ya habari.
“Hatuna
wasiwasi na vyombo vya habari tunataka viendelee kuwepo ila view vinafuata
maadili.
“Uhuru
wa vyombo vya habari sio kutangaza habari yoyote huo utakuwa sio uhuru wa
habari bali hiyo ni vumai ya habari,”alisema.
Rais
Kikwete, alisema hawatakubali kuona baadhi ya vyombo vya habari vinatumia uhuru
huo vibya kwa kutangaza habari za uchezi, chuki na vuruma katika jamii.
‘Lakini
ukisema serikali ya CCM imeshindwa hilo halina madhara na siwa,”alisema Rais
Kikwet.
Akizungumzia
Azam Media, Rais Kikwete, aliutaka uongozi wa kampuni hiyo kujikita zaidi
katika kuwapatia mafunzo wafanyakazi wake ili waweze kwenda mabadiliko ya
kiteknolojia.
Alisema
kwa kufanya hivyo kutawasaidia kuwa na wafanyakazi wenyeueledi na bora zaidi
kiutendaji.
“Mafunzo
ni muhimu kwenye kazi kinyume chake mtakuata utendji wao wote unashuka na
watakuwa wakitoa habari mbaya,”alisema.
Pia
Rais Kikwete, alisistiza suala mishahara kwa wafanya kazi wao kama
hawakuliangalia hilo watambue kuwa watalipwa mitaani kitendo kitakachowafanya
watowe habari za hao waliowapa.
Rais
Kikwete, alipongeza uongozi wa Azam kwa kujenga studio ambayo alisema hajapata
kuiona katika ukanda huu.
Mtendaji
Muu wa Azam Group, Saidi Bakhresa, alisema haikuwa rashisi kukamilisha mradi
huo kwani ilikuwa ni shughuli pevu.
Alisema
kikubwa anaishukuru serikali kwa kutoa fursa sawa katika uwekezaji, ambapo pia
aliwashukuru Watanzania kwa kuwaunga mkono katika matumizi ya bidhaa zao.
Naibu Mtendaji Mkuu wa Azam Media Group, Tido
Mhando, alisema Studio hiyo ni yakisas,
ambayo italeta mapinduzi katika utangazaji wa televisheni nchini.
“Studio zetu ni za kisasa zaidi ndani ya
Afrika Mashariki na Kati, labda tunaweza kuzifananisha na studio za BBC, CNN au
Al Jazeera.
“Tunataka
kuhakikisha tunaleta mapinduzi ya utangazaji wa television nchini hasa katika
suala la michezo, wapenzi wa michezo wategemee mambo makubwa kutoka kwetu,” alisema
Mhando.
Azam TV imekua
ikionesha moja kwa moja (live) mechi zote za ligi kuu Tanzania bara na
wanatarajia kuboresha matangazo hayo ya mpira ili kuwapa burudani zaidi wapenzi
wa michezo huo nchini na nchi zote ambako matangazo ya Azam TV yanafika.
No comments:
Post a Comment