MKE wa Rais, Mama Salma Kikwete amewataka
wanawake kutambua kuwa kujikwamua kwao kiuchumi kutaanza ndani ya nafsi zao
wenyewe.
Sambamba na hilo, baadhi ya wanawake wa kawaida
wamesema hawaitambui siku hiyo ya wanawake duniani.
Mama Kikwete alitoa kauli hiyo, wakati wa kilele
cha maadhimisho ya Siku ya Mwanamke Duniani kwa Mkoa wa Dar es Salaam,
iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazimmoja jijini jana.
Alisema kujikwamua huko kutatokana na dhamira
sahihi na ya dhati ya mhusika kuheshimu kila fursa anayoipata na kuanzia hapo
atakuwa amejifungulia milango ya mafanikio.
“Wanawake wa Mkoa wa Dar es Salaam katika
Risala yenu mmeongea masuala mbalimbali mazuri.
“Kuhusu changamoto ya mikopo yeneye riba nafuu,
serikali kupitia Mfuko wa kuendeleza wanawake na Vijana inaendelea kutoa mikopo
hiyo kupitia Halmashauri za Manispaa za Mkoa huu,”alisema Mama Salma.
Mama Kikwete alisema katika mwaka wa fedha 2014/15, Halmashauri zote tatu za mkoa huo zimetenga
jumla ya sh bilioni 1.50 (1,050,000,000).
Alisema wilaya ya Ilala imetenga sh milioni
500, Kinondoni sh. milioni 250 na Temeke
sh milioni 300 .
Kutoka na fedha hizo zilizotengwa kwa ajili ya
wanawake na vijana, anawashauri watumie fursa hiyo ya mikopo iliyopo katika
ngazi ya halmashauri kujiletea maeneleo.
Katika kumkwamua mwanamke, itakumbukwa kuwa
mwaka 2012 aliwahi kuzindua mpango kasi wa uwezeshaji wa wanawake na wasichana
na Desemba 2014 alizindua mpango mwingine wa kuzuia mimba za utotoni.
Mama Salma, alisema lengo lilikuwa ni
kuwawezesha wasichana kuendelea na masomo tangu elimu ya msingi hadi chuo
kikuu.
Alitoa wito kwa wanawake kuendelea na juhudi za
kujikomboa kielimu na kiuchumi kwa kujishughulisha na shughuli mbalimbali za
ujasiriamali, kujiunga na vikundi vya kiuchumi vilivyoko katika maeneo yao kama
vile vya VICOBA na vinginevyo vya kuweka na kukopa.
Aidha, Mama Kikwete, alisema wanawake wa mkoa
huo wameendelea kukuathirika zaidi ikiwemo maradhi kama vile, Ukimwi, vifo
vinavyotokana na uzazi ambavyo vinaweza kuzuilika.
Athari nyingine ni unyanyasaji wa kijinsia,
kubakwa, mimba za utotoni na kunyimwa haki ya kumiliki mali hususan ardhi.
“Hivyo, basi maadhimisho hayo si kwa ajili ya
kufanya sherehe tu, pia ni kufanya tathimini kwa pamoja kutafakari namna gani
tumepiga hatua katika kukabiliana na changamoto hizo,”alisema Mama Kikwete.
Alisema
baada ya kutafakari wazijadili na
kutafuta mbinu na mikakati bora zaidi katika kumkomboa mwanamke na changamoto
hizo.
Wanawake
wa Kawaida
Wanawake wa kawaida baadhi yao wamesema
hawaitambui siku hiyo, wanachojua ni yawanawake wanaofanyakazi maofisini.
Tatu Daud ambaye ni mfanyabiashara ya kuuza
vitafunwa eneo la Posta mpya alisema pamoja na kuwako viongozi wanawake lakini
hawajajitokeza katika kukemea manyanyaso wanayofanyiwa na mgambo wa jiji kwa
kukanyagakanyaga biashara zao.
Alisema serikali imewatenga, hawndewi haki
wananyanyaswa, wanafukuzwa viumbe vyenye madhara kila wanapojaribu kutafuta
kipato kwa siku hii ni ya maombolezo kwetu.
Hadija Mwalimu, alisema serikali inawashauri
wakope mikopo ili wajikwamue kiuchumi lakini cha kushangaza serikali hiyo
inawazuia wasifanye biashara katika maeneo ambayo yanawateja wao.
“Tunakamatwa na askari wa jiji na kwenda
kulipishwa faini y ash 50,000 wakati hata mtaji tuliokopa ni sh 20,000 kweli
utasema wanawake tunathaminiwa na ukiangalia fedha hizo ndio tunazitegemea
kulisha familia na kupeleka watoto wetu shule na mambo mengine,”alisema Hadija.

No comments:
Post a Comment