WAZIRI
Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye amesema kuwa taifa linahitaji kuwa na amani na
utulivu wakati wa uandikishaji wa wapiga kura katika daftari la wapiga kura,
wakati wa kampeni , pamoja na wakati wa kutangaza matokeo.
Sumaye aliyasema hayo jana Tabora Mjini wakati
wa harambee ya ujenzi wa Kanisala Moravian Tanzania Magharibi, wilaya ya Reli
ya Kati Tabora, ambapo alisema kuwa
katikia mwaka huu ni muhimu uchaguzi uandaliwe vizuri, ufanyike kwa haki na
uwazi na usimamiwe vizuri.
Alisema
lengo la uchaguzi ni kupata viongozi wapya wazuri, waadilifu, wapenda na watenda
haki na wachapa kazi kwani hayo ndio mambo ya msingi yanayowafanya watu
wamwombe Mungu nyakati za chaguzi maana nchi nyingi zimeingia kwenye misukosuko
kwa kutokuwa makini nyakati za chaguzi.
“Tunahitaji
kumwomba Mungu wetu sana ili uchaguzi wetu upite salama na utuletee viongozi
watakaojali maslahi ya watu na siyo maslahi yao binafsi au ya marafiki zao wa
karibu. Katika jambo hili kuna mambo kadhaa muhimu ya kufanya kazi, likiwemo
kuliombea taifa na kuwa na amani na utulivu,”alisema.
Akizungumzia
kuhusu amani, Sumaye amesema kuwa lazima serikali ihakikishe kwa
kushirikiana na Tume ya Uchaguzi (NEC) kuwa raia wote wenye kustahili kupiga
kura wanaandikishwa katika daftari rasmi la wapiga kura.
Aidhama,
nafasi ya kutosha itolewe ili kila mtu apate hiyo fursa ya kuandikishwa kupiga
kura. Ni muhimu daftari hilo likawa wazi kwa kila mtu kukagua jina lake na
kituo chake cha kupigia kura ili kusiwe na malalamiko ya watu kutokuona majina
yao au majina kuwa katika vituo vingine ambavyo haviko karibu nao.
“Pia
wakati wa Kampeni Tume ihakikishe kuwa vyama vyote vinapewa haki sawa na wote
wanalindwa na sheria na taratibu zilizowekwa. Vyombo vya dola vihakikishe
kampeni ni za utulivu na fujo zozote zinadhibitiwa na wavunja amani
wanaadhibiwa bila kujali umaarufu wao wala wa vyama wanakotoka,”alisema.
Alisema
hatua hiyo inatokana na kushuhudiwa watu wakienda kwenye mikutano ya kampeni na
silaha za moto au za jadi hali ambayo inasababisha watu kukatwa mapanga,
mashoka na nondo.
“Vyama
vya siasa vinatakiwa viwaelimishe watu wao kuwa siasa si uadui wala mapambano
ya silaha bali ni kushindana kwa hoja. Vyombo vya dola katika eneo hili
vinatakiwa vifanye kazi bila huruma mradi vinafuata sheria.
Sote tukumbuke kuwa
hakuna chama chochote wala kiongozi yeyote aliye juu ya sheria,”alieleza.
Kuhusu
udanganyifu katika kuhesabu kura na kutangaza matokeo, Sumaye alisema kuwa hilo
ni eneo nyeti na kama uwazi wa kutosha haupo fujo na umwagaji damu huweza
kutokea.

No comments:
Post a Comment