KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday, 8 March 2015

VIJANA NCCR WAMPENDEKEZA DK KAHANGWA AGOMBEE URAIS

KITENGO cha Vijana wa Chama cha NCCR Mageuzi, kimempendekeza Dk. George Kahangwa kuwa mgombea wa nafasi ya urais katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Uwamuzi wa Kitengo hicho haumzui mwanachama mwingine wa chama hicho kujitokeza na kuomba kugombea nafasi hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini leo kwa niaba ya vijana wenzake, Mwenyekiti wa kitengo hicho, Deo Meck amesema wamefikia umauzi huo baada ya kufanya utafiti wa muda mrefu ndani ya chama kuhusu mgombea anayefaha.

Amesema, kutokana na mazoea kwamba wagombea wa nafasi mbalimbali hujitokeza wao wenyewe, lakini kitengo hicho kimekuwa tofauti baada ya kushiriki kumtafuta mgombea urais atakaye peperusha bendera ya chama na kuliletea taifa mabadiliko chanaya.

“Tuliona tutafute mtu anayekidhi vigezo vya kutosha vya kikatiba, mwenye sifa zinazotajwa na chama ambazo ni uwezo, ucha mungu, kuchukia ufisadi na awe mzalendo asiyetiliwa shaka,”alisema.
Amesema kwamba mbali ya kumuomba agombee, pia wanamtaka akubaliane na pendekezo lao la kumchukulia fomu ya chama na kumlipia ada inayotakiwa pindi wakati utakapowadaia.

Halladhalika wameshindwa kupendekeza jina la Mwenyekiti wa chama hicho James Mbatia, kwa vile tayari amekwisha tangaza nia ya kugombea ubunge katika Jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro.

“Tutafanya jitihada na kuhakikisha jina lake linafika katika kikao cha Halmashauri ya chama, ili lipewe baraka za mkutano mkuu wa chama, hatimaye kushindanishwa na wagombea wengine watakaosimamishwa na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kuwa mgombea wa ngazi ya urais,”alisema.

Akitaja wasifu wa Dk.Kahangwa amesema ni Mhadhiri wa 
Chuo Kikuu Dar es Salaam kampasi ya Mlimani, ambaye anafanya tafiti kufundisha na kutoa huduma kwa jamii katika masuala ya uongozi, sera na mipango hususan ya elimu.

“Alipata shahada yake ya kwanza chuoni hapo mwaka 2004, ambapo alipata ufaulu wa juu na kuibuka mwanafunzi bora wa kitivo, pia alihitimu mafunzo ya uongozi katika taasisi ya Kijerumani iitwayo Fredrich Ebert Stiftung (FES),”.

Mbali na hayo ni mhitimu wa shahada ya uzamivu (udakltari falsafa), katika Chuo cha Briston Uingereza, pamoja na kusomea masuala ya kimataifa katika chuo cha Oulu nchini Finland.

Kuhusu uzoefu wa kisiasa, Dk.Kahangwa aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa chama hicho ngazi ya Taifa, Mkuu wa Idara ya Itikadi, Sera na Mafunzo pamoja na kuwa Makamu Mkuu wa chuo cha chama.

Alitaja sifa zilizochangia kumpendekeza Dk.Kahangwa,  amesema wamezingatia umri, elimu, uzalendo na kashfa za kisiasa ndio maana wamempendekeza.

“Hakuwahi kuwa na kashfa yoyote ya kisiasa ni msafi hana hata doa, pia kiwango chake cha elimu kipo juu, hata hivyo ana uzalendo na uwezo wa kuliongoza taifa licha ya kuwa hana umaarufu wa kutisha,”amesema.

Hata hivyo, amesema kwamba hawamnyimi nafasi mwanachama yoyote anayetaka kuwania nafasi hiyo, kwani uamuzi walioufanya wao ni kupendekeza mgombea wakiwa kama vijana waliokuwa ndani ya chama.

No comments:

Post a Comment