KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday, 17 March 2015

WABAHA'i KUSHEREHEKEA NAW-RUZ


NA MWANDISHI WETU

JUMUIYA ya Wabaha’i jijini Dar es Salaam wanaungana na Wabaha’i wengine ulimwenguni kusherehekea mwaka wao mpya (Naw-Ruz).
 Ofisa Mwenezi   wa  Baraza la Kiroho la Mahali Wabaha’i wa Dar es Salaam, Qudsiyeh Roy, alisema jana kuwa sherehe hizo zitafanyika Machi 21, mwaka huu, Baha’I Senta, iliyopo Mtaa wa Mfaume, Upanga, Dar es Salaam.

Alisema katika sherehe hizo kutakuwa na mkusanyiko wa ibada  na kwamba sala za Kibaha’i zitasomwa katika lugha mbalimbali.

Naw-Ruz katika imani ya Baha’i ni mojawapo ya siku takatifu tisa kwa wafuasi wa imani hiyo ya  Baha’i ulimwenguni kote na siku ya kwanza ya kalenda ya Baha’i.


Siku hiyo ya Naw-Ruz hufuata mwezi wa Kibaha’i wa mfungo. Mwaka wa Kibaha’i una miezi  19 na siku 19. Katika mwezi wa mfungo, Wabaha’i husali na kutafakari na hujitahidi kurekebisha tabia yao, kutakasa mioyo yao na kufikia daraja la juu zaidi la kujitenga na mambo ya dunia. 

No comments:

Post a Comment