BAADHI ya
Wasanii wamesema wamepoteza kamu ya muziki kutokana na kifo cha Kepteni Komba, kilichotokea
katika Hospitali ya TMJ jijini Dar es Salaam juzi, kilichosababishwa maradhi ya
kisukari..
Kauli hiyo
ilitolewa na wasanii hao jana wakati walipokwenda nyumbani kwa marehemu Kepteni
Komba Mbezi Beach jijini Dar es Salaam kutoa pole kwa ndugu wa marehem.
Walisema hivyo,
kwa vile Komba alikuwa msanii wa pekee ambaylikuwa na uwezo wa kutunga nyumbo
za matukio pindi yanapotokea ghafla.
Ummy Wenceslaus
(Dokii), alisema Kepteni Komba alikuwa mtu ambaye aliwasaidia wasanii wengi
ambao baadhi yao walifanikiwa akiwemo Ramadhan Masanja (Banza Stone).
“Alikuwa ni mtu
mwenyekipaji mwenye sauti nzuri na yapekee, alikuwa anasikiliza watu alikuwa
akitoa ushauri kwa kila aliyekuwa akitaka kukamilisha malengo yake,”alisema
Dokii.
Dokii, alisema
wamepoteza mpiganaji wa kweli katika fani kwani alikuwa chapa kazi na kwamba
alikuwa akijiamni katika maamuzi yake.
Naye Rais wa
Shirikisho la Muziki wa Nyimbo za Injili, (Shimuta), Ado Novemba, alisema
alikuwa mtu wa ajabu kwani kutokana na madaraka aliyokuwa nayo angekuwa
kiongozi mwingine angeacha kupiga muziki lakini kwake ilikuwa tofauti.
Aidha, walisikitishwa na baadhi ya watu wanaotoa
taarifa mbaya kuhusu marehemu, kwa kweli siyo vizuri, na watambue kuwa marehemu
hana makosa.
No comments:
Post a Comment