WATOTO 11,000 hulazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kila mwaka kutokana na kushambuliwa na ugonjwa upungufu wa damu mwilini (Siko Seli).
Mratibu wa Kitengo cha Siko Seli, Dk Robert Mongi, alisema hayo wakati
akipokea msaada wa simu 150 za mkononi kwa ajili ya kuratibu matibabu ya wagonjwa wanaotibiwa
kwenye kitengo hicho.
Simu hizo zilizotolewa na kampuni ya simu za mkononi Vodacom kupitia
taasisi yake ya kusaidia masuala ya
jamii ya Vodacom Foundation.
Alisema tatizo la ugonjwa huo
kwa watoto ni kubwa nchini na limekuwa likiongezeka kila mwaka na kusababisha
watoto wengi kulazwa.
Hata hivyo, Dk. Mongi alisema ugonjwa huo unatibika iwapo mgonjwa atapima na kuanza
kutumia dawa mapema ikiwemo kuzingatia
“Vipimo vya ugonjwa huo vinapatikana katika hospitali ya Taifa ya
Muhimbili tu, hali ambayo inasababisha waathirika wa ugonjwa huu wanaoishi nje
ya mkoa wa Dar es Salaam
kuchelewa kupata vipimo na wengi wao kupoteza maisha,”alisema Dk. Mongi.
Alisema kutokuwepo mashine za kupima ugonjwa huo za kutosha ni moja
ya changamoto kubwa inayokwamisha kuutokomeza ugonjwa huo nchini.
Aidha, Dk. Mongi aliishukuru Vodacom Foundation kwa
msaada huo ambao utawafikia walengwa hususan wagonjwa wanaotumia dawa pia
zitwasaidia katika huduma nyingine muhimu kiafya.
Meneja wa Ruzuku na Mawasiliano wa Vodacom Foundation Renatus
Rwehikiza alisema kampuni ya Vodacom kupitia taasisi yake hiyo imeona kuna umuhimu wa kuwapatia wagonjwa simu ili
ziwasaidie wakati wa matibabu yao.
“Tunajua kuwa kuna makundi mengi ya wahitaji katika jamii hivyo
tumeona safari hii tuangalie kundi la wagonjwa
wanaotibiwa Siko Seli kwa kuwa ugonjwa huu unazidi kuongezeka na
unahitaji jitihada za ziada kutoka kwa wadau mbalimbali katika kuutokomeza”.Alisema
Rwehikiza.

No comments:
Post a Comment