![]() |
| Mwenyekiti wa Baraza la Wakulima (ACT), Dk Sinare. |
Mwenyekiti wa Baraza hilo, Dk. Sinare Sinare,
alisema Baraza hilo limefikia hatua hiyo baada ya kufanya majadilino na
kukiandikia barua chama hicho cha siasa mwaka huu kubadili kifupisho hicho, lakini
hadi sasa chama hicho kinaonekana kudharau matakwa ya baraza hilo.
Alisema dharau hizo za (ACT-Tanzania), zimesababisha kuleta
mkanganyiko kwa wanachama wa baraza la kilimo kushindwa kutofautisha baadhi ya
taarifa zinazotokana na vifupisho vya Baraza na chama hicho.
“Kinachotokea ni wanasiasa kutopenda kufuata sheria, wao
walichotakiwa kwanza ni kufuatilia kwenye mitandao ambako wangegundua uwepo wa
jina lenye kifupisho chetu,”alisema Dk. Sinare.
Dk. Sinare, alisema baraza hilo,
limefikia uamuzi wa kukitaka chama hicho kuacha kutumia kifupicho hicho kwa
vile baraza limeanzishwa tangu mwaka 1999 na kupata setifiketi ya kumiliki nembo
hiyo ya ACT ya mwaka 2014.
“Haiwezekani katika nchi moja kuwa na taasisi mbili tofauti zinazotumia
nembo moja inayofanana na kwa yeyote atakayekwenda kinyume kwa kutumia nembo
hiyo kwa maslahi tofauti na baraza watambuwe kuwa upo uwezo wa kuburuzwa katika
vyombo vya sheria,”alisema Dk. Sinare.

No comments:
Post a Comment