KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Monday, 6 April 2015

ASKOFU PENGO AWALILIA WAKENYA WALIYOUWAWA GARISSA


Askofu, Pengo

ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Karidinal Pengo, amesema mashambulizi ya yaliyofanywa na kikundi cha kigaidi cha Al Shabab katika Chuo Kikuu cha Garissa nchini Kenya yamewatia hofu Wakristo.

 Askofu Pengo alisema hayo wakati ibada ya misa takatifu iliyofanyika katika Palokia ya kipawa na kuwakutanisha wanakwaya wa kanisa hilo jijini Dar es Salaam leo.

Alisema, mauaji ya baadhi ya wakristro yaliyotokea katika Chuo Kikuu cha Garissa, hakuna mtu aliyeamini kwamba vikundi hivyo vibaya vingevamia na  kuanza kuwauwa wakristu.

Askofu Pengo, alisema jambo hilo limewatia hofu na wasiwasi mkubwa kwani hawakuwahi kufikiria hata siku moja  kama vitendo hivyo vya kigaidi vingeweza kutokea.

“Nawaomba niwaulize hivyi nani aliamini kuwa Kenya wangeweza kuvamiwa tena na kikundi cha kuvunja amani na kuchagua wakristo na waislamu kisha kuwauwa wakristo, hali hii inatisha sana na kusikitisha kama  sasa wanaanza kuuwawa watu kutokana na dini zao,” alisema.

Askofu Pengo alisema zamani vita ya watu wa Kenya ilikuwa makabila kwa makabila  lakini sasa imekuwa tofauti imeingia katika dini hivyo wakristu wanauwawa pasipo na hatia katika nchi yao.

“Tulijua kuwa Kenya wanagombana kwa makabila lakini kwamba wataanza kuulizwa wewe ni mkristu unapigwa risasi ila mwiislamu anachwa huru, hili ni jambo la hatari inatubidi kumuomba sana mwenyezi Mungu atuepushe na balaa hilo lakini pia tuiombee nchi ya

Kenya iwe na amani,” alisema.
Hata hivyo Askofu Pengo aliwataka waamini wa kikristo kuwa na ujasiri wa kubaiki na msimamo kwa kutoiga dini ya wengine kwa kuogopa kuuliwa na kumuommba mungu awaimarishe na kudumu kwenye imani yao huku wakikumbuka utukufu wa Bwana Yesu.

No comments:

Post a Comment