![]() |
| Mhandisi Bonaventure Baya |
BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi
wa Mazingira (NEMC), limewataka wazalishaji, waingizaji, wasambazi, na wauzaji
mifuko ya plastiki (Rambo), kujiorodhesha, watakaoshindwa kutekeleza agizo hilo watachukuliwa hatua
za kisheria.
Tangazo hilo
limekuja baada ya Baraza hilo
kubaini kuwa matumizi ya mifuko hiyo licha ya kupigwa marufuku, yamekuwa
yakiongezeka kila kukicha.
Agosti mwaka 2013 serikali kupitia
aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (mazingira), Dk. Terezya
Huvisa, ilipiga marufuku wazalishaji, waingizaji, wasambazi, wauzaji na
utumiaji wa mifuko hiyo ya plastiki.
Wakati huo, Dk. Huvisa alikaririwa na
vyombo vya habari akisema kuwa jitihada zinahitajika ili kuhakikisha kuwa
marufuku hiyo inazingatiwa, msako wa watu wanaofanyabiashara hiyo unafanyika
katika maeneo yote ndani ya nchi na watakaokiuka sheria wachukuliwe hatua.
Madhara yanayosababishwa na mifuko ya
plastiki ni pamoja na uharibifu wa udongo unaotokana na kuunguzwa kwa plastiki
hizi na hivyo kusababisha madhara ya kiafya kwa binadamu na wanyama ,kutooza
kiurahisi wa njia za kiasili (non-biodegradable) kuzagaa katika mito, maziwa,
bahari na nchi kavu hivyo kuhatarisha maisha ya viumbe hai wanaoishi katika
mazingira.
Hata hivyo, tangu kipindi hicho mifuko hiyo
imekuwa ikiendelea kutumika katika maeneo mbalimbali ya nchi tena bila kificho.
Katika tangazo lake alilolitoa kwenye
vyombo vya vya habari, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Bonaventure Baya,alisema kazi
hiyo ya kujiandikisha itafanyika katika Ofisi za Baraza hilo, ziliziko makao
makuu Dar es Salaam au zile zilizoko Mbeya, Mwanza, Arusha na Mtwara miezi kwa miezi miwili kuanzia Aprili Mosi
hadi Mei 30 mwaka huu.
Kwa mujibu wa NEMC, hatua hiyo ni
kutimiza matakwa ya sheria ya usimamizi wa mazingira namba 20 ya mwaka 2004 na
kanuni ya mifuko ya plastiki ya mwaka 2006.
“Usajili huu ni muhimu sana katika kusaidia maamuzi ya namna ya
kushughulikia tatizo la mifuko hii ya plastiki nchini,”alisema.
Baya, alisema kuwa watakaoshindwa
kujiorodhesha ifikapo Mei 30 watambue kuwa shughuli zao zitasimamishwa na
kuchukuliwa hatua za kisheria
“Tunaujulisha umma kuwa wazlishaji kuwa
wazalishaji, waingizaji, wauzaji wa jumla na watumiaji wakubwa wa mifuko ya
plastiki wote nchini, mfano Supermarket mnatakiwa kujiorodhesha katika ofisi
zetu za NEMC tilizowajulisha,”alisema.
Baraza linaendelea kusistiza kuwa kwa
mujibu wa kanuni ya mifuko ya plastiki ya mwaka 2006, mifuko inayoruhusiwa
kisheria ni ile yenye unene wa kuanzia mikroni 30 na yote inayotumika au
kuzalishwa nchini kuwa ni lazima iwe na alama (Nembo), ya mzalishaji au
muagizaji.

No comments:
Post a Comment