| Kulia ni MSAJILIWA Msaidizi wa Vyama vya Siasa nchini Sisty Nyahoza akimkabidhi Mwenyekiti wa CKUT, Ramadhan Semtawaa cheti cha usajili wa muda. |
SAJILIWA Msaidizi wa Vyama
vya Siasa nchini Sisty Nyahoza amesema chama cha siasa ili kifanye vizuri
kinahitaji kuwa na misingi ya utawala bora, baadae kifikie malengo yake ya
kushika dola.
Miongoni mwa misingi hiyo ni
pamoja na kuwa na Katiba yenye misingi ya kidemokrasia.
Nyahoza, alisema hayo, jijini
leo wakati akikabidhi cheti cha usajili wa muda kwa Mwenyekiti wa Chama cha
Kijamaa na Uzalendo Tanzania (C.K.U.T), Ramadhan Semtawa.
Alisema, kila chama kina
hitajika kujenga demokrasia ya kweli ambayo ni muhimu hususan ikaanza ndani ya
chama kwani itawasaidia viongozi kufikia
malengo waliyojiwekea.
Nyahoza, alisema viongozi pia
wanawajibu wa kusoma sheria ya vyama vya sisasa ili kuepuka migongano na
watendaji wa taasisi zingine za serikali.
“Leo tumetoa cheti cha
usajili wa muda kwa chama cha CKUT, tunawaomba sana viongozi wa chama hiki
kukaa pamoja na wanachama wenu ili kupeana mawazo mazuri ya kujenga chama.
“Asitokee mmoja miongoni
mwenu akadai kuwa yeye ndiye mwenye chama, nawashauri someni vizuri sheria ya
vyama ili kuepuka mgogoro na taasisi zingine,” alisema.
Naye Msajili wa Vyama vya
Siasa, Mstaafu Jaji Francis Mutungi, alisema ofisi ya msajili ni taasisi maalum
na iko pale kwa ajli ya kuwahudumia watu wote wanaohitaji huduma kama hiyo.
Mwenyekiti wa chama hicho cha
CKUT Semtawa, alisema wameanzisha chama kwa malengo maalumu ya kurejesha nchi
kwenye misingi ya waasisi ambao walijali haki za wanyonge.
Alisema, nchi imetawaliwa na rushwa
kila kona jambo ambalo limewafanya wananchi wanyonge wakose haki zao.
Semtawa, alisema kutokana
mazingira hayo CKUT, kitakapoingia madarakani kitahakikisha kuwa kina rudisha
nchi katika misingi ya kidemokrasia na utawala bora.
“Watu wanauwa kwa sababu za
kidini na wengine upoteza maisha yao kwa imani za kishirikina, lakini pia wapo
watu wamekuwa wakila fedha za serikali na hawachukuliwi hatua yoyote, tunataka
kuja kuibadilisha nchi hii maana aina muelekea kwa sasa,” alisema.
Semtawa alisema kazi kubwa
iliyoko mbele yao ni kutafuta wanachama ili waweze kupata usajili wa kudumu
jambo ambalo anaamini kuwa litafanikiwa.
“Tunatakiwa tuwe na wanachama
2000 katika mikoa kumi na kila mkoa mmoja inatubidi tupate wanachama 200,
tumejipanga vizuri na tunaamini kuwa tutapata usajili wa kudumu,”alisema.
Aidha, Semtawa alisema hawatahitaji
kiongozi yoyote kutoka katika vyama vya upinzani kujiunga na chama hicho kwa
vile kufanya hivyo kutapunguza nguvu ya upinzani.
Alisema chama hicho kiko
tayari kupokea viongozi wasafi kutoka CCM, ambao hawakubaliani na vitendo vichafu
vinavyofanywa na wenzao wasiozingatia maadili ndani ya chama hicho.
“Hatutawapokea tu bali
tutawachunguza kwanza mienendo yao tangu wakiwa ndani ya chama hicho na hata
uadilifu wao nje ya chama,”alisema Semtawa.
No comments:
Post a Comment