WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, amewataka Watanzania kuilinda amani kwani ndio inawafanya wawe kitu kimoja
Lowassa, alitoa kauli hiyo, wakati wa Siku ya Ibada ya Ijumaa Kuu, iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Usharika wa Azania Front, jijini Dar es Salaam juzi.
Alisema ni jambo la kumshukuru mungu kwamba nchi kuwa inasherehekea siku hiyo ya Ijumaa Kuu ikiwa na amani na utulivu.
Lowassa, alisema kutokana na mazingira hayo, Watanzania wanapaswa kuienzi amani iliyoasisiwa na waasisi, kwani bila ya amani wasingeweza kusherehekea siku hiyo wakiwa pamoja.
No comments:
Post a Comment