KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday, 5 April 2015

SUMAYE AWATAKA WATANZANIA KUIMARISHA ULINZI NA USALAMA WA NCHI


Waziri Mkuu wa zamani, Sumaye

WAZIRI Mkuu wa zamani Fredrick Sumaye amewataka Watanzania kuimarisha ulinzi na usalama wa nchi ili kuepuka mashambulizi ya kigaidi kama yale yanayotokea Kenya.

Siku nne zilizopita nchini Kenya kumetokea mashambulizi ya kigaidi katika Chuo Kikuu cha Garissa, yaliyofanywa na Kikundi cha Al Shabab, ambayo hadi sasa yanasadikiwa kuwa yameua zaidi ya watu 147.

Sumaye, alitoa kauli hiyo wakati wa ibada ya ibada ya Siku ya Ijumaa Kuu, iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Azania Front, jijini Dar es Salaam juzi.

Alisema hivyo kwa vile wapo baadhi ya Watanzania wanaodhani kuwa mashambulizi kama yale hayawezi kutokea nchini wakiamini Tanzania ni nchi ya amani.

Sumaye, alisema ili nchi iweze kuwepukana na mashambulizi kama yale  ni lazima kila mmoja kuwa makini na watu wanaowatilia mashaka na kuacha dhana kwamba suala la ulinzi ni la polisi au majeshi pekee.

“Tumeona hivi karibuni kuna kikundi cha watu kilijificha kwenye mapango ya amboni na kuaanza kutishia amani ya nchi yetu, sasa ni lazima watanzania tujenge umoja wa na tuwafichuwe watu hao wenye nia mbaya ya kuvuruga amani yetu,”alisema Sumaye.

Licha ya mashambulizi nchini Kenya bado hapa nchini kuna matatizo ya baadhi ya vituo vya polisi kuvamiwa na baadhi ya polisi kuuawa na kuporwa silaha jambo ambalo linapaswa kuchukuliwa hatua za haraka ili kulikomesha.

Akizungumzia Ujumbe wa siku hiyo, Sumaye, alisema watanzania wanapaswa kuonyesha upendo kwa baadhi ya watu wanaokabiliwa na matatizo.

Alisema hata Yesu aliteswa msalabani kwa ajili ya upendo wa kuwasaidia wanadamu hivyo ni vema kwa kila mmoja kuepuka kuanzisha misuguano kama vile mivutano ya wafugaji na wakulima.

No comments:

Post a Comment