![]() |
| Mbunge wa Moshi Mjini, Ndesamburo |
MBUNGE wa Moshi mjini Philemon
Ndesamburo ameitaka serikali kuweka mfumo wa kamera ambao utakaosaidia
kudhibiti madereva wanaokwenda kinyume na sheria za usalama barabarani na
kusababisha vifo vya Watanzania wasikuwa na hatia.
Ndesamburo, alitoa kauli hiyo baada ya
kuisikia taarifa kwenye vyombo vya habari kuwa serikali imeondoa utaratibu wa
tochi barabarani kwa vile ulikuwa ni miongoni mwa madai ya madereva wakati
walipogoma wiki iliyopita.
Katika mgomo huo madereva walikuwa
wakidai kuwa wamechoka kufanyakazi bila ya mikataba inayoeleweka, kutolipwa
mishahara na wengine kulipwa kwa utaratibu wa huduma za simu jambo ambalo
linaikosesha mapato serikali.
Kingine ni utaratibu wa tochi wawapo
safarini, kikubwa ambacho wanapinga ni utaratibu wa kutakiwa kwenda kusoma tena
kila baada ya miaka mitatu wanapobadilisha leseni zao ambapo pia walidai kuwa
ada ya sh. 560, 000 ya mafunzo hayo ni kubwa, kwamba wao ni vibarua hawana
uwezo wa kupata fedha hizo.
Wakati akijibu kero za madereva hao juzi
Waziri, alisema kuwa serkali imeyapokea matatizo yao na kwamba utaratibu wa
kurudia kusoma umefutwa, tochi barabarani hakuna na vituo vituo vya ukaguzi
vitatumika vya mizani tu.
Akizungumza na mwandishiwa habari
hizi, kwa njia ya simu, Mbunge huyo alisema hakubaliani na uamuzi wa kuondolewa
tochi barabarani kwani kwa kufanya hivyo ajali zitaongezeka zaidi.
“Tanzania watu wanakufa kila siku
kutokana na madereva kwenda mbio, sasa huyo waziri kuondoa tochi unadhani
atapunguza ajali au watu waendelee kufa? Sasa huyo waziri kuondoa tochi ina
mana anataka watu waendelee kufa, mimi sikubaliani naye,”alisema Ndesamburo.
Alisema hivyo kwa mfumo wa tochi
umeshindwa kufanyakazi kutokana na wasimamizi wake kuugeuza mfumo huo kuwa
mradi wa rushwa barabarani hivyo kupoteza imani kwa madereva.
Alisema mfumo huo watochi
umelalamikiwa kutokana na waliokabidhiwa dhamana kushindwa kuwatendea haki
madereva hivyo kuufanya uonekane kuwa haufai.
Ndesamburo alisema kutokana na mazingira
hayo ni vema serikali ikaanzisha mfumo wa kamera ambao unatumika katika nchi mbalimbali
zilizoendelea.
“Naamini utaratibu wa kuweka kamera
unawezekana, nchi hii fedha zipo, kama watu walijichotea fedha za Escrow walivyotaka
iweje washindwe kuweka kamera, inawezekana kabisa,”alisema Nesamburo.
Kuhusu elimu, Ndesamburo alisema elimu
haina mwisho na ndio maana hata wazee leo wanasoma, hivyo hakubaliani na
uwamuzi wa kufuta mafunzo ya madereva, kwa vile ulimwengu wa sasa ni wa sayansi
na teknolojia hivyo kunakuwa na madiliko ya mara kwa mara katika matumizi ya
vyombo mbalimbali katika kila sekta.
Alisema ziandaliwe sheria ambazo zitaleta tija kwa walengwa huku kila tajiri ambaye ameamua kuajiri akubali kulipa gharama za mafunzo ya dereva wake, wazingatie kwamba elimu ni msingi wa kila kitu duniani.

No comments:
Post a Comment