WAZIRI
Mkuu, Mizengo Pinda, amesema Watanzania waishio ughaibuni hawataweza kupiga
kura wakiwa nje ya nchi kwenye uchaguzi wa Oktoba mwaka huu.
Pinda
alitoa kauli hiyo juzi alipozungumza na baadhi ya Watanzania waishio Uingereza
kwenye makazi ya Balozi wa Tanzania
nchini humo, Balozi Peter Kallaghe, yaliyoko Highgate, Kaskazini mwa Jiji la London.
Alisema
mambo makuu yanayohitaji kuzingatiwa kabla hawajaweza kupiga kura ni
marekebisho ya sheria ya uchaguzi namba 1 ya mwaka 1985 pamoja na uandikishwaji
wa Watanzania wana-Diaspora kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
"Najua
suala kubwa ambalo mnatamani kulisikia ni hili la Watanzania kuweza kupiga kura
kutokea huku mliko. Hili inawezekana lisifanikiwe wakati huu kwa sababu kuna
mambo muhimu ya kuzingatia kubwa likiwa ni marekebisho ya sheria.
“Pia ili
mwananchi aweze kupiga kura ni lazima awe ameandikishwa kwenye Daftari la
Kudumu la Wapigakura," alisema.
Alisema
wanaangalia kama mashine za BVR nazo zitapaswa kupelekwa kwenye kila ubalozi,
ili watu waweze kujiandikisha au itafutwe njia nyingine ya kufanikisha hilo jambo.
“...
lakini watu wa tume wanaamini kwamba jambo hilo linaweza kufanikiwa kwenye uchaguzi wa
mwaka 2020," alisema.
Waziri
Mkuu ambaye aliwapatia nakala zisizopungua 40 za Katiba Inayopendekezwa,
alitumia fursa hiyo kuwasisitizia wasome kwa makini Katiba hiyo ili wawe na
uelewa mpana.

No comments:
Post a Comment