![]() |
| Mwenyekiti wa TLP, Mrema |
MPASUKO
ndani ya Chama cha TLP umejitokeza baada ya Mwenyekiti wa chama hicho Agaustino
Mrema kuwalazimisha Wajumbe wa Mkutano Mkuu waliokuwa wakipinga uteuzi wa Katibu
Mkuu wa Chama, Nancy Mlikaria, wa mkubali.
Mpasuko
huo umekuja baada ya wajumbe hao kupinga kitendo cha katibu mkuu wa anayemaliza
muda wake kuteuliwa tena na mwenyekiti wa chama hicho huku akiwa mgombea pekee.
Jana alfajiri
katika Ukumbi wa Crystal Palace, Sinza jijini Dar es Salaam, wandishi wa habari ilishuhudia
wajumbe hao wakimpinga mwenyekiti wao waziwazi kutokana na uwamuzi wake wa
kibabe wakuwataka wajumbe lazima wamkubali katibu huyo.
Mmoja wa
wajumbe hao ambaye alianza kuzunguza bila ya kutaja jina, kutoka kanda ya Ziwa alisema
katibu huyo hafai kwa vile hawezi kwenda sambamba na kasi ya ushindani wa vyama
vingi.
Alisema,
kuwa katibu huyo wanampinga kutokana na tabia zake za kutokuwa na ushirikiano
mzuri na wanachama walioko katika ofisi za chama huko mikoani.
Mjumbe
kutoka Mkoa wa Mara, alimuonya mwenyekiti kuwa kitendo chake cha kutaka
arudishwe katika nafasi hiyo, atambuwe kuwa yatakapokuja kutokea yakutokea basi
atambuwe kutakuja kuwajibika kutokana na natatizo ya katibu huyo.
Mvutano
huo wa kumkubali au kumtaa ulichukuwa zaidi ya saa 1 hadi pale Mwenyekiti wa
chama, Mrema, alipowaomba wajumbe wa mkubali kwa kumpima kwa kipindi cha miezi
sita.
Pamoja na
ombi hilo la Mrema
bado wajumbe hao waliendelea na msimamo wao wa kumkataa katibu huyo, hali
iliyomfanya mwenyekiti huyo kutishia kuvunja mkutano huo.
Kauli hiyo
ilitafsiriwa wajumbe wenyeuzoefu na tabia za mwanyekiti huyo, kuwa kama kweli angevunja mkutano huo basi asinge wapa posho
kitendo ambacho kingewaletea usumbufu wa kurudi makwao.
Hata
hivyo, kabla ya wajumbe hao kujibu, Mrema aliagiza kwa kusema wanaomkubali Nancy wanyooshe mkono juu,
hali iliyo wafanya wengi kunyoosha, ikiashiria kuwa wamemkubali.
Baada ya
kupitishwa kwa mbinde, Mrema alimuonya katibu huyo kuwa amesikia alivyolalamikiwa
sasa ni wajibu wake wa kubadilika na kwamba hata kubali kuona anaiendesha ofisi
ya chama anavyotaka.
Nancy, alisema kuwa changamoto zote
amezisikia akiahidi kuzifanyia kazi hususan kwa kushirikiana na wanachana wote.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Ukweli na Maridhiano ya chama hicho, James Haule, alisema
kilichofanyika ni kikao cha kupeana taarifa na si uchaguzi mkuu.
Alisema
kwa taratibu za uchaguzi ilitarajiwa kabla ya uchaguzi ilitakiwa achaguliwe
mwenyekiti wa muda kwa ajili ya kusimamia uchaguzi huo.
Haule
alisema baada hatua mbalimbali za uchaguzi kukamilika mwenyekiti huyo wa muda
ndio angetangaza matokeo.
“Kwa
mujibu wa kanuni za uchaguzi wa chama mwenyekiti wa uchaguzi ndio anatangaza
matokeo hata kukiwa na mgombea mmoja hata kama
amepigiwa kura ya hapana au ndio,”alisema Haule.
Alisema,
hayo yote hayakufanyika na kilichojitokeza ni Mrema, kusimamia shughuli zote za
uchaguzi mwanzo hadi mwisho.
Aidha,
alisema kuna wananchama waliozuiliwa kugombea nafasi ya mwenykiti kwa kwa lengo
la kumfanya Mrema amekosa mpinzani.
Alisema
mwanachama aliyezuiwa kwa madai kuwa amechelewa kurudisha fomu ni Mutamwega
Mugaihwa, wakati sio kweli na cha kushangaza wapo waliokubaliwa kuchukua fomu
hadi juzi asubuhi siku ya mkutano huo.
Hata
hivyo, chama hicho kilikuwa hakijatangaza matokeo rasmi kutokana uchaguzi huo
kumalizika jana alfajiri.
MWISHO

No comments:
Post a Comment